< Otra Ķēniņu 18 >
1 Un Hosejas, Elas dēla, Israēla ķēniņa, trešā gadā Hizkija, Ahaza, Jūda ķēniņa, dēls, palika par ķēniņu.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Un viņš bija divdesmit pieci gadus vecs, kad palika par ķēniņu, un valdīja divdesmit deviņus gadus Jeruzālemē, un viņa mātei bija vārds Abi, Zaharijas meita.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
3 Un tas darīja, kas Tam Kungam labi patika, tāpat kā viņa tēvs Dāvids bija darījis.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
4 Tas nopostīja tos kalnu altārus un nolauzīja tos stabus un izdeldēja Astartes un sadragāja to vara čūsku, ko Mozus bija taisījis; jo līdz tam laikam Israēla bērni tai bija kvēpinājuši un to nosauca Neūstan (vara taisīta).
Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
5 Viņš uzticējās Tam Kungam, Israēla Dievam, un pēc viņa nebija otrs tāds kā viņš no visiem Jūda ķēniņiem, arī priekš viņa tāds nebija bijis.
Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
6 Jo viņš pieķērās Tam Kungam un viņš no Tā neatkāpās un viņš turēja tos baušļus, ko Tas Kungs caur Mozu bija pavēlējis.
Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
7 Un Tas Kungs bija ar viņu, ka viss, kur viņš izgāja, labi izdevās. Viņš atkāpās arīdzan no Asīrijas ķēniņa un tam vairs nekalpoja.
Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
8 Viņš kāva arīdzan Fīlistus līdz Gazai un viņas robežām, gan pilīs, gan stiprās pilsētās.
Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
9 Un ķēniņa Hizkijas ceturtā gadā, tas ir Hosejas, Elas dēla, Israēla ķēniņa, septītais gads, Salmanasers, Asīrijas ķēniņš, cēlās pret Samariju un apmeta lēģeri pret viņu.
Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
10 Un to uzņēma pēc trim gadiem, Hizkijas sestā gada, tas ir Hosejas, Israēla ķēniņa, devītais gads, - tad Samarija tapa uzņemta.
Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
11 Un Asīrijas ķēniņš aizveda Israēli uz Asīriju un tiem lika dzīvot Halahā un pie Haboras, Gozanas upes, un Medijas pilsētās,
Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
12 Tāpēc ka tie Tā Kunga, sava Dieva, balsij nebija klausījuši, bet viņa derību pārkāpuši, un visu, ko Mozus, Tā Kunga kalps, bija pavēlējis, un to nebija nedz klausījuši nedz darījuši.
Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
13 Bet ķēniņa Hizkijas četrpadsmitā gadā Sanheribs, Asīrijas ķēniņš, cēlās pret visām stiprām Jūda pilsētām un tās uzņēma.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
14 Tad Hizkija, Jūda ķēniņš, sūtīja pie Asīrijas ķēniņa uz Laķisu un lika sacīt: es esmu apgrēkojies, griezies atpakaļ no manis, es nesīšu, ko tu man uzliksi. Tad Asīrijas ķēniņš Hizkijam, Jūda ķēniņam, uzlika trīssimt talentus sudraba un trīsdesmit talentus zelta.
Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
15 Un Hizkija deva visu sudrabu, kas atradās Tā Kunga namā un tā ķēniņa nama mantās.
Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
16 Tanī laikā Hizkija noplēsa (to zeltu) no Tā Kunga nama durvīm un no tiem stabiem, ko Hizkija, Jūda ķēniņš, bija apkalis ar zeltu, un to deva Asīrijas ķēniņam.
Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
17 Bet Asīrijas ķēniņš sūtīja Tartanu (augsto sargu), Rabsarisu (augsto valdoni) un Rabzaku (augsto dzērienu devēju) no Laķisas pie ķēniņa Hizkijas ar lielu karaspēku uz Jeruzālemi, un tie cēlās un gāja uz Jeruzālemi. Un kad tie bija cēlušies un nonākuši, tad tie nostājās pie augšēja dīķa ūdens grāvja, ceļa malā pie vadmalnieku tīruma.
Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
18 Un tie sauca ķēniņu. Tad pie tiem izgāja nama uzraugs Elijaķims, Hilķijas dēls, un skrīveris Šebna un kanclers Joaks, Asafa dēls.
Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
19 Un Rabzakus uz tiem sacīja: sakāt jel Hizkijam: tā saka tas lielais ķēniņš, Asīrijas ķēniņš: kas tas tāds patvērums, uz ko tu paļaujies?
Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
20 Tu saki tukšu vārdu, diezgan esot padoma un spēka uz karu. Uz ko tad tu paļaujies, ka tu no manis esi atkritis?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
21 Nu redzi, tu paļaujies uz to salūzušo niedri, uz Ēģipti. Kas uz to atspiežas, tam tā ies rokā un to pārdurs. Tāds ir Faraons, Ēģiptes ķēniņš, visiem, kas uz viņu paļaujas.
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
22 Bet ja jūs uz mani sakāt: mēs paļaujamies uz To Kungu, savu Dievu: vai tas nav, kam kalnus un altārus Hizkija ir nopostījis un sacījis uz Jūdu un Jeruzālemi: priekš šī altāra, kas ir Jeruzālemē, jums būs pielūgt?
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
23 Nu tad, noderi ar manu kungu, Asīrijas ķēniņu, un es tev došu divtūkstoš zirgus, ja tev ir jātnieki, ko tiem likt virsū.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
24 Kā tad tu varēsi atsist atpakaļ vienu pašu virsnieku no mana kunga vismazākiem kalpiem? Bet tu paļaujies uz Ēģipti, ratu un jātnieku dēļ.
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
25 Vai tad nu es bez Tā Kunga esmu cēlies pret šo vietu, to izpostīt? Tas Kungs uz mani sacījis: celies pret šo zemi un izposti to.
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
26 Tad Elijaķims, Hilķijas dēls, un Šebna un Joaks sacīja uz Rabzaku: runā jel ar saviem kalpiem sīriski, - mēs to gan protam - un nerunā ar mums jūdiski priekš šo ļaužu ausīm, kas ir uz mūra.
Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
27 Bet Rabzakus uz tiem sacīja: vai mans Kungs mani sūtījis pie tava kunga un pie tevis, šos vārdus runāt? Vai ne pie tiem vīriem, kas sēž uz mūra, kam līdz ar jums būs jāēd savi sūdi un jādzer savi mīzali.
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
28 Un Rabzakus nostājās un sauca ar stipru balsi jūdiski un runāja un sacīja: klausāties tā lielā ķēniņa, Asīrijas ķēniņa, vārdus.
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
29 Tā saka ķēniņš: lai Hizkija jūs neapmāna, jo viņš jūs nevarēs izglābt no manas rokas.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
30 Lai arī Hizkija jums nedara cerību uz To Kungu sacīdams: tiešām, Tas Kungs mūs izglābs un šī pilsēta netaps dota Asīrijas ķēniņa rokā.
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
31 Neklausāties uz Hizkiju. Jo tā saka Asīrijas ķēniņš: deriet ar mani mieru un nāciet pie manis ārā, tad ikviens ēdīs no sava vīna koka un ikviens no sava vīģes koka un ikviens dzers ūdeni no savas akas,
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
32 Kamēr es nākšu un jūs aizvedīšu tādā zemē, kāda ir jūsu zeme, labības un vīna zeme, maizes un vīna dārzu zeme, eļļas koku, eļļas un medus zeme, - tad jūs paliksiet dzīvi un nemirsiet. Bet Hizkijam neklausiet, jo viņš jūs pieviļ sacīdams: Tas Kungs mūs izpestīs.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
33 Vai gan pagānu dievi ikviens savu zemi izglābuši no Asiriešu ķēniņa rokas?
Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
34 Kur ir Hamatas un Arpadas dievi? Kur ir Sefarvaimas, Enas un Ivas dievi? Vai tie gan izglābuši Samariju no manas rokas?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
35 Kurš no visas pasaules dieviem izglābis savu zemi no manas rokas? Kā tad Tas Kungs Jeruzālemi izglābs no manas rokas?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
36 Bet tie ļaudis cieta klusu un viņam neatbildēja neviena vārda, jo ķēniņš bija pavēlējis un sacījis: jums nebūs viņam atbildēt.
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
37 Tad nama uzraugs Elijaķims, Hilķijas dēls, un skrīveris Šebna un kanclers Joaks, Asapa dēls, nāca pie Hizkijas ar saplēstām drēbēm un viņam stāstīja Rabzakus vārdus.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.