< Otra Ķēniņu 12 >

1 Jeūs septītā gadā Joas palika par ķēniņu un valdīja četrdesmit gadus Jeruzālemē. Un viņa mātei bija vārds Cibea no Bēršebas.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 Un Joas darīja, kas Tam Kungam labi patika, visu savu mūžu, kamēr priesteris Jojada viņu mācīja.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 Tikai kalnu altāri netapa nopostīti; jo tie ļaudis upurēja un kvēpināja vēl uz tiem kalnu altāriem.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 Un Joas sacīja uz tiem priesteriem: visu naudu, kas top dota Dievam par godu un nāk Tā Kunga namā, naudu, kas iet uz galvām, visu naudu, ko spriež par dvēseli, un visu naudu, ko dod no labprātības Tā Kunga namā,
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 To priesteriem būs ņemt, ikkatram no sava pazīstama, un tiem būs izlabot tā nama plīsumus visur, kur tie plīsumus atrod.
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 Un notikās ķēniņa Joasa divdesmit un trešā gadā, ka tie priesteri nebija labojuši tā nama plīsumus,
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 Tad ķēniņš Joas aicināja priesteri Jojadu un tos citus priesterus un uz tiem sacīja: kāpēc jūs nelabojiet tā nama plīsumus. Un nu jums vairs nebūs ņemt naudu no saviem pazīstamiem, bet to dot priekš tā nama plīsumiem.
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 Tad tie priesteri bija mierā, naudas no ļaudīm vairs neņemt, nedz nama plīsumus izlabot.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 Un priesteris Jojada ņēma šķirstu un ieurba tā vākā caurumu, un to lika sānis altārim pa labo roku; kad kāds nāca Tā Kunga namā, tad tie priesteri, kas slieksni sargāja, tur ielika to naudu, ko ienesa Tā Kunga namā.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 Kad nu redzēja daudz naudas šķirstā esam, tad ķēniņa skrīveris un augstais priesteris nāca un sasēja un skaitīja to naudu, ko atrada Tā Kunga namā.
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 Un tie to naudu ieskaitīja rokā darba uzraugiem, kas bija iecelti pār Tā Kunga namu. Un tie to izdeva amatniekiem un nama būvētājiem, kas pie Tā Kunga nama strādāja,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 Un mūrniekiem un akmeņu cirtējiem, pirkt kokus un cirstus akmeņus, izlabot Tā Kunga nama plīsumus un izdot par visu, kas bija vajadzīgs, izlabot Tā Kunga namu.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 Bet sudraba kausus, nažus, bļodas, trumetes un visādas zelta un sudraba lietas priekš Tā Kunga nama netaisīja no tās naudas, ko sanesa Tā Kunga namā,
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 Bet tie to deva strādniekiem, izlabot ar to Tā Kunga namu.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 Un atbildēšanu neprasīja no tiem vīriem, kam tā nauda bija dota, to dot strādniekiem, bet tie to darīja uz ticību.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 Nauda no noziegumu upuriem un nauda no grēku upuriem netapa nesta Tā Kunga namā, tā nācās priesteriem.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 To brīdi Azaēls, Sīriešu ķēniņš, cēlās un karoja pret Gatu un to uzņēma. Un Azaēls griezās iet pret Jeruzālemi.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 Tad Joas, Jūda ķēniņš, ņēma visas svētās dāvanas, ko viņa tēvi Jehošafats un Jehorams un Ahazija, Jūda ķēniņi, Dievam bija dāvinājuši, ir tās dāvanas, ko viņš pats bija devis, un visu zeltu, kas atradās Tā Kunga namā un pie ķēniņa nama mantām, un to sūtīja Azaēlim, Sīriešu ķēniņam. Tad šis aizgāja no Jeruzālemes.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 Un kas vēl par Joasu stāstāms, un viss, ko viņš darījis, tas ir rakstīts Jūda ķēniņu laiku grāmatā.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 Un viņa kalpi cēlās un derēja derību un nokāva Joasu Millus namā, kur iet uz Sillu.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 Jo Jozakars, Šimeata dēls, un Jozabats, Šomera dēls, viņa kalpi, to nokāva, ka tas nomira; un viņu apraka pie viņa tēviem Dāvida pilī. Un viņa dēls Amacīja palika par ķēniņu viņa vietā.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< Otra Ķēniņu 12 >