< Otra Ķēniņu 10 >

1 Un Ahabam bija septiņdesmit dēli Samarijā, un Jeūs rakstīja grāmatas un tās sūtīja uz Samariju pie Jezreēles virsniekiem, pie tiem vecajiem un Ahaba bērnu uzraugiem ar šiem vārdiem:
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 Kad šī grāmata pie jums nonāk, un jūsu kunga dēli ir pie jums, un rati un zirgi, stipra pilsēta un bruņas,
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 Tad izredziet to labāko un taisnāko no sava kunga dēliem, un ieceļat to viņa tēva goda krēslā, un karojiet par sava kunga namu.
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 Bet tie bijās varen ļoti un sacīja: redzi, divi ķēniņi viņa priekšā nav pastāvējuši, kā tad mēs pastāvēsim?
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 Un kas par to namu un pilsētu bija iecelts, un tie vecaji un uzraugi sūtīja pie Jeūs un sacīja: mēs esam tavi kalpi un darīsim visu, ko tu mums sacīsi, mēs nevienu necelsim par ķēniņu; dari tu, kas tev patīk.
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 Tad viņš tiem rakstīja citu grāmatu ar šiem vārdiem: ja jūs esat manā pusē un gribat klausīt manai balsij, tad ņemiet sava kunga dēlu galvas un nāciet pie manis rīt ap šo laiku uz Jezreēli. (Un to ķēniņa dēlu bija septiņdesmit vīri pie pilsētas lielkungiem, kas tos audzināja.)
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 Kad nu šī grāmata pie tiem atnāca, tad tie ņēma tos ķēniņa dēlus un nokāva visus septiņdesmit un lika viņu galvas kurvjos un tās sūtīja uz Jezreēli.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 Un kad tas vēstnesis atnāca un viņam to stāstīja sacīdams: tie ir atnesuši ķēniņa dēlu galvas, tad viņš sacīja: lieciet tās divējās kopās pie vārtu durvīm līdz rītam.
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 Un no rīta, kad viņš izgāja, tad viņš tur nostājās un sacīja uz visiem ļaudīm: jūs esat taisni, redzi, es esmu cēlis dumpi pret savu kungu un viņu nokāvis; kas tad šos visus ir kāvis?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Tāpēc atzīstiet, ka no Tā Kunga vārda nekas nav kritis zemē, ko Tas Kungs runājis pret Ahaba namu; jo Tas Kungs ir darījis, ko Viņš runājis caur savu kalpu Eliju.
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 Tad Jeūs arī visus apkāva, kas no Ahaba nama bija atlikušies Jezreēlē, arī visus viņa augstniekus un viņa pazīstamos un viņa svētītājus, kamēr tam neviena vairs neatlika.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 Un viņš cēlās un gāja un nonāca Samarijā un bija ceļā vienā namā, kur gani dzīvoja.
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 Tad Jeūs atrada Ahazijas, Jūda ķēniņa, brāļus un uz tiem sacīja: kas jūs esat? Un tie sacīja: mēs esam Ahazijas brāļi un esam nākuši apmeklēt ķēniņa un ķēniņienes bērnus.
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 Tad viņš sacīja: grābiet tos dzīvus. Un tie tos sagrāba dzīvus un tos apkāva pie ganu nama akas, četrdesmit un divus vīrus, un neatlicināja no tiem neviena.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 Un no turienes aizgājis viņš atrada Jonadabu, Rekaba dēlu, pretī nākam, un to apsveicināja un uz to sacīja: vai tava sirds taisna, kā mana sirds ar tavu sirdi? Un Jonadabs sacīja: ir gan. (Jeūs sacīja: ) Ja tā ir, tad dod man savu roku. Un viņš tam deva roku. Un viņš tam lika pie sevis kāpt ratos.
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 Un viņš sacīja: nāc man līdz un skaties manu karstumu priekš Tā Kunga. Un viņš tam lika braukt savos ratos.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 Tad viņš nonāca Samarijā un apkāva visus, kas Ahabam bija atlikuši Samarijā, tiekams viņš tos izdeldēja, pēc Tā Kunga vārda, ko tas caur Eliju bija runājis.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 Un Jeūs sapulcināja visus ļaudis un uz tiem sacīja: Ahabs Baālam maz ir kalpojis, Jeūs viņam daudz vairāk kalpos.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 Tāpēc aicinājiet visus Baāla praviešus, visus viņa kalpus un visus viņa svētītājus pie manis, ka neviens neatraujās, jo man Baālam jaupurē liels upuris. Nevienam, kas atraujās, nebūs palikt dzīvam. Bet Jeūs to darīja ar viltību, ka viņš nomaitātu visus Baāla kalpus.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 Un Jeūs sacīja: svētījiet Baālam svētkus, un tie tos izsauca.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 Tad Jeūs sūtīja arī pa visu Israēli, un visi Baāla kalpi atnāca, un neviens neatrāvās, kas nebūtu nācis, un tie nāca Baāla namā, ka Baāla nams līdz galu galam bija pilns.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 Tad viņš sacīja uz tiem, kas bija iecelti pār to drēbju namu: atnesiet visiem Baāla kalpiem drēbes, un tie viņiem atnesa drēbes.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 Tad Jeūs ar Jonadabu, Rekaba dēlu, gāja Baāla namā, un viņš sacīja uz Baāla kalpiem: meklējiet un pieraugāt, ka jūsu starpā nav neviena no Tā Kunga kalpiem, bet Baāla kalpi vien.
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 Kad tie nu nāca upurēt kaujamos un dedzināmos upurus, tad Jeūs ārā nolika astoņdesmit vīrus un sacīja: ja kāds no tiem vīriem, ko es jums dodu rokā, izbēgs, tad jūsu dvēsele būs viņa dvēseles vietā.
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 Kad nu dedzināmais upuris bija pabeigts, tad Jeūs sacīja uz pils karavīriem un uz virsniekiem: ejat un kaujiet tos, ka neviens neizbēg. Un tie tos apkāva ar zobena asmeni, un tie pils karavīri un virsnieki tos nometa pie malas un gāja Baāla nama pilī.
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 Un tie iznesa Baāla nama uzceltos stabus un tos sadedzināja,
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 Un sadragāja Baāla uzcelto tēlu un salauzīja Baāla namu un to darīja par gānekļu vietu līdz šodienai.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 Tā Jeūs Baālu izdeldēja no Israēla.
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 Bet no Jerobeama, Nebata dēla, grēkiem, kas Israēli bija pavedis uz grēkiem, Jeūs neatstājās, proti no tiem zelta teļiem Bētelē un Danā.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 Un Tas Kungs sacīja uz Jeū: “Tāpēc ka tev labs prāts bijis darīt, kas Man patīk un Ahaba namam visu esi darījis, kas bija Manā sirdī, tad tavi dēli tev sēdēs Israēla krēslā līdz ceturtam augumam.”
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 Bet Jeūs nedzinās staigāt Tā Kunga, Israēla Dieva, bauslībā ar visu savu sirdi; viņš neatstājās no Jerobeama grēkiem, kas Israēli bija pavedis uz grēkiem.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 Tanī laikā Tas Kungs Israēli iesāka mazināt, jo Azaēls tos kāva visās Israēla robežās,
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 No Jardānes puses pret rītiem visu Gileādas zemi, Gadiešus un Rūbeniešus un Manasiešus, no Aroēra pie Arnonas upes un Gileādu un Basanu.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 Un kas vēl par Jeū stāstāms, un viss, ko viņš darījis, un viss viņa spēks, tas ir rakstīts Israēla ķēniņu laiku grāmatā.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 Un Jeūs aizmiga saviem tēviem pakaļ un viņu apraka Samarijā, un viņa dēls Joakas palika par ķēniņu viņa vietā.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 Un tas laiks, kamēr Jeūs pār Israēli valdījis Samarijā, ir divdesmit un astoņi gadi.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< Otra Ķēniņu 10 >