< Otra Laiku 23 >
1 Bet septītā gadā Jojada iedrošinājās un cēla derību ar tiem virsniekiem pār simtiem, Azariju, Jeroama dēlu, un Ismaēli, Johanana dēlu, un Azariju, Obeda dēlu, un Maāseju, Adajas dēlu, un Elizavatu, Sihrus dēlu.
Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.
2 Un tie gāja pa Jūdu apkārt un sapulcināja Levitus no visām Jūda pilsētām un Israēla tēvu namu virsniekus, un tie sanāca Jeruzālemē.
Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu,
3 Un visa draudze derēja derību Dieva namā ar ķēniņu, un viņš uz tiem sacīja: redzi, ķēniņa dēlam būs būt par ķēniņu, tā kā Tas Kungs runājis par Dāvida dēliem.
kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu. Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi.
4 To nu jums būs darīt: Trešdaļa no jums, kam svētdienā krīt kārta, no priesteriem un Levitiem, lai vakti tur pie durvīm.
Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni,
5 Un trešdaļa lai stāv ķēniņa namā, un trešdaļa pie Pamatu vārtiem. Un visi ļaudis lai stāv Tā Kunga nama pagalmā.
theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana.
6 Bet nevienam nebūs Tā Kunga namā ieiet, kā vien priesteriem un Levitiem, kas kalpo; tie var ieiet, jo tie ir svēti, bet visi ļaudis lai tur Tā Kunga vakti.
Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana.
7 Un Leviti lai stājās visapkārt ap ķēniņu, ikkatrs ar savu ieroci rokā, un kas namā ieiet, tam būs mirt, bet jums būs būt pie ķēniņa, kad tas ieiet un iziet.
Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
8 Un Leviti un visa Jūda valsts darīja pēc visa, ko priesteris Jojada bija pavēlējis, un ikviens ņēma savus vīrus, kam svētdienā krita kārta un kam svētdienā kārta beidzās. Jo priesteris Jojada tiem kārtniekiem neļāva aiziet.
Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke.
9 Un priesteris Jojada deva tiem virsniekiem pār simtniekiem šķēpus un priekšturamās bruņas un tās bruņas, kas ķēniņam Dāvidam bijušas, kas bija Dieva namā.
Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu.
10 Un viņš nostādīja visus ļaudis, ikvienu ar savu ieroci rokā, no nama labās puses līdz nama kreisai pusei, līdz altārim un namam visapkārt ap ķēniņu.
Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
11 Un tie izveda to ķēniņa dēlu un viņam uzlika kroni un tam deva to liecības grāmatu un to cēla par ķēniņu. Un Jojada ar saviem dēliem to svaidīja un sacīja: lai dzīvo ķēniņš!
Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
12 Kad nu Atalija to ļaužu kliegšanu dzirdēja, kas bija saskrējuši un ķēniņu slavēja, tad viņa nāca pie tiem ļaudīm Tā Kunga namā.
Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana.
13 Un tā skatījās, un redzi, ķēniņš stāvēja savā vietā pie durvīm un lielkungi un taurētāji bija pie ķēniņa, un visi zemes ļaudis priecājās un pūta trumetes, un dziedātāji ar saviem rīkiem pavadīja tās slavas dziesmas. Tad Atalija saplēsa savas drēbes un sacīja: dumpis, dumpis!
Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”
14 Bet priesteris Jojada lika iziet tiem virsniekiem pār simtiem, tiem kara vadoņiem, un uz tiem sacīja: izvediet to ārā no nama caur rindām, un kas viņai ies pakaļ, to būs ar zobenu nokaut. Jo tas priesteris bija sacījis: nenokaujiet to Tā Kunga namā.
Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.”
15 Un tie tai deva ceļu atkāpdamies uz abējām pusēm, un kad tā ieejot pa tiem zirgu vārtiem nāca ķēniņa namā, tad tie viņu tur nokāva.
Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.
16 Un Jojada derēja derību starp sevi un visiem ļaudīm un ķēniņu, ka tie būtu Tā Kunga ļaudis.
Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana.
17 Tad visi ļaudis gāja Baāla namā un to nolauzīja un viņa altārus, un sadauzīja viņa bildes un nokāva Matanu, Baāla priesteri, altāru priekšā.
Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.
18 Un Jojada iecēla atkal par uzraugiem pie Tā Kunga nama priesterus, tos Levitus, ko Dāvids bija atšķīris Tā Kunga namam, upurēt Tam Kungam dedzināmos upurus, kā Mozus bauslībā rakstīts, ar prieku un ar dziesmām pēc Dāvida likuma.
Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza.
19 Un viņš iecēla vārtu sargus pie Tā Kunga nama vārtiem, ka neviens tur neieietu, kas kaut kādas lietas dēļ nešķīsts.
Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.
20 Un viņš ņēma tos virsniekus pār simtiem un varenos un ļaužu lielkungus, arī visus zemes ļaudis, un noveda ķēniņu no Tā Kunga nama un gāja caur augšējiem vārtiem ķēniņa namā, un sēdināja ķēniņu uz valstības krēslu.
Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi,
21 Un visi zemes ļaudis priecājās, un pilsēta norima pēc tam, kad Ataliju bija nokāvuši ar zobenu.
nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.