< Pirmā Laiku 5 >

1 Un Rūbena, Israēla pirmdzimušā dēla, bērni, (jo viņš bija tas pirmdzimušais, bet tāpēc, ka tas bija sagānījis sava tēva gultu, viņa pirmdzimtība tapa dota Jāzepa, Israēla dēla, bērniem, bet to tik neskaitīja (cilts rakstos) par pirmdzimto.
Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
2 Jo Jūda palika varens starp saviem brāļiem, un no viņa bija tas valdnieks, bet Jāzepam palika tā pirmdzimtība).
Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
3 Rūbena, Israēla pirmdzimušā dēla, bērni bija: Hanoks un Palus, Hecrons un Karmus.
Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
4 Joēļa bērni bija: Šemajus, tā dēls Gogs, tā dēls Šimejus,
Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
5 Tā dēls Miha, tā dēls Reaja, tā dēls Baāls,
Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
6 Tā dēls Beēra, ko TiglatPilnesers, Asīrijas ķēniņš, aizveda cietumā, - tas bija Rūbena bērnu lielskungs.
na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
7 Un viņa brāļi pēc saviem radiem, kā tie savos radu rakstos tapa skaitīti: virsnieks Jejels un Zaharija,
Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
8 Un Belus, Asasa dēls, tas bija Zemas, tas Joēļa dēls, tas dzīvoja Aroērā un līdz Nebum un BaālMeonam;
Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
9 Un pret rītiem viņš dzīvoja, līdz kamēr nāk tuksnesī pie Eifrat upes, jo viņu ganāmie pulki bija vairojušies Gileādas zemē.
Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
10 Un Saula laikā tie karoja pret Agariem; un šie krita caur viņu rokām, un tie dzīvoja viņu teltīs visā Gileādas rīta pusē.
Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
11 Un Gada bērni dzīvoja tiem pretī Basanas zemē līdz Zalkai.
Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
12 Joēls tas pirmais un Safans tas otrais un Jaēnajus un Šafats Basanā.
Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
13 Un viņu brāļi pēc viņu tēvu namiem bija: Mikaēls un Mešulams un Zebus un Jorajus un Jaēkans un Zija un Hebers, septiņi.
Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
14 Šie bija Abikaīļa bērni, tas bija Ura, tas Jarvas, tas Gileāda, tas Mikaēļa, tas Jezizajus, tas Jādas, tas Busa dēls.
Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
15 Akus, Abdiēļa dēls, Gunas dēla dēls, bija virsnieks pār viņu tēvu namu.
Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
16 Un tie dzīvoja Gileādā un Basanā un viņu piederīgās vietās un visā Šarona apgabalā līdz viņu galiem.
Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
17 Visi šie tapa sazīmēti radu rakstos Jotama, Jūda ķēniņa, laikā, un Jerobeama, Israēla ķēniņa, laikā.
Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
18 Rūbena bērnu un Gada bērnu un Manasus puscilts, kas bija sirdīgi vīri un bruņas un zobenu nesa un stopu uzvilka un uz karu mācīti, to bija četrdesmit četri tūkstoši septiņsimt sešdesmit, kas gāja karā.
Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
19 Un tie karoja pret Agariem un Jeturu un Navesu un Nodabu.
Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
20 Bet tiem nāca palīgs pret šiem, un Agari tapa doti viņu rokā un visi, kas ar tiem bija. Jo tie piesauca Dievu kaujā, un viņš no tiem likās pielūgties, tāpēc ka tie uz viņu cerēja.
Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
21 Un tie noveda lopus, piecdesmit tūkstoš kamieļus, divsimt piecdesmit tūkstoš avis un divtūkstoš ēzeļus un simt tūkstoš cilvēkus.
Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
22 Jo daudz krita ievainoti, tāpēc ka tā kauja bija no Dieva. Un tie dzīvoja viņu vietā līdz cietuma laikam.
na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
23 Un Manasus puscilts bērni dzīvoja tai zemē un vairojās no Basanas līdz Baāl Hermonam un Senirai un Hermona kalnam.
Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
24 Un šie bija viņu tēva namu virsnieki: Hefers un Jezejus un Eliēls un Asriēls un Jeremija un Odavija un Jakdiēls, stipri varoņi, slaveni vīri, savu tēvu nama virsnieki.
Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
25 Bet kad tie apgrēkojās pret savu tēvu Dievu un maukoja pakaļ to zemes ļaužu dieviem, ko Dievs viņu priekšā bija izdeldējis,
Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
26 Tad Israēla Dievs pamodināja Pūla, Asīrijas ķēniņa, garu un Tiglat-Pilnesera, Asīrijas ķēniņa, garu un aizveda cietumā Rūbena bērnus un Gada bērnus un Manasus puscilti un tos noveda uz Alu un Aboru un Aru un pie Gozanas upes līdz šai dienai.
Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.

< Pirmā Laiku 5 >