< Psalmorum 96 >

1 quando domus aedificabatur post captivitatem canticum huic David cantate Domino canticum novum cantate Domino omnis terra
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 cantate Domino benedicite nomini eius adnuntiate diem de die salutare eius
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 adnuntiate inter gentes gloriam eius in omnibus populis mirabilia eius
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 quoniam magnus Dominus et laudabilis valde terribilis est super omnes deos
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 quoniam omnes dii gentium daemonia at vero Dominus caelos fecit
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 confessio et pulchritudo in conspectu eius sanctimonia et magnificentia in sanctificatione eius
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 adferte Domino patriae gentium adferte Domino gloriam et honorem
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 adferte Domino gloriam nomini eius tollite hostias et introite in atria eius
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 adorate Dominum in atrio sancto eius commoveatur a facie eius universa terra
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 dicite in gentibus quia Dominus regnavit etenim correxit orbem qui non movebitur iudicabit populos in aequitate
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 laetentur caeli et exultet terra commoveatur mare et plenitudo eius
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 gaudebunt campi et omnia quae in eis sunt tunc exultabunt omnia ligna silvarum
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 a facie Domini quia venit quoniam venit iudicare terram iudicabit orbem terrae in aequitate et populos in veritate sua
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Psalmorum 96 >