< Psalmorum 91 >

1 laus cantici David qui habitat in adiutorio Altissimi in protectione Dei caeli commorabitur
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
2 dicet Domino susceptor meus es tu et refugium meum Deus meus sperabo in eum
Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
3 quoniam ipse liberabit me de laqueo venantium et a verbo aspero
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4 in scapulis suis obumbrabit te et sub pinnis eius sperabis
Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5 scuto circumdabit te veritas eius non timebis a timore nocturno
Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
6 a sagitta volante in die a negotio perambulante in tenebris ab incursu et daemonio meridiano
wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7 cadent a latere tuo mille et decem milia a dextris tuis ad te autem non adpropinquabit
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
8 verumtamen oculis tuis considerabis et retributionem peccatorum videbis
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
9 quoniam tu Domine spes mea Altissimum posuisti refugium tuum
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10 non accedent ad te mala et flagellum non adpropinquabit tabernaculo tuo
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
11 quoniam angelis suis mandabit de te ut custodiant te in omnibus viis tuis
Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
12 in manibus portabunt te ne forte offendas ad lapidem pedem tuum
Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13 super aspidem et basiliscum ambulabis et conculcabis leonem et draconem
Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
14 quoniam in me speravit et liberabo eum protegam eum quia cognovit nomen meum
Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
15 clamabit ad me et exaudiam eum cum ipso sum in tribulatione eripiam eum et clarificabo eum
Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
16 longitudine dierum replebo eum et ostendam illi salutare meum
Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”

< Psalmorum 91 >