< Psalmorum 87 >
1 filiis Core psalmus cantici fundamenta eius in montibus sanctis
Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 diligit Dominus portas Sion super omnia tabernacula Iacob
Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
3 gloriosa dicta sunt de te civitas Dei diapsalma
Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
4 memor ero Raab et Babylonis scientibus me ecce alienigenae et Tyrus et populus Aethiopum hii fuerunt illic
“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
5 numquid Sion dicet homo et homo natus est in ea et ipse fundavit eam Altissimus
Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
6 Dominus narrabit in scriptura populorum et principum horum qui fuerunt in ea diapsalma
Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 sicut laetantium omnium habitatio in te
Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”