< Psalmorum 80 >
1 in finem pro his qui commutabuntur testimonium Asaph psalmus qui regis Israhel intende qui deducis tamquam oves Ioseph qui sedes super cherubin manifestare
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 coram Effraim et Beniamin et Manasse excita potentiam tuam et veni ut salvos facias nos
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Deus converte nos et ostende faciem tuam et salvi erimus
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Domine Deus virtutum quousque irasceris super orationem servi tui
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 cibabis nos pane lacrimarum et potum dabis nobis in lacrimis in mensura
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 posuisti nos in contradictionem vicinis nostris et inimici nostri subsannaverunt nos
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Deus virtutum converte nos et ostende faciem tuam et salvi erimus
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 vineam de Aegypto transtulisti eiecisti gentes et plantasti eam
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 dux itineris fuisti in conspectu eius et plantasti radices eius et implevit terram
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 operuit montes umbra eius et arbusta eius cedros Dei
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 extendit palmites suos usque ad mare et usque ad Flumen propagines eius
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 ut quid destruxisti maceriam eius et vindemiant eam omnes qui praetergrediuntur viam
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 exterminavit eam aper de silva et singularis ferus depastus est eam
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Deus virtutum convertere respice de caelo et vide et visita vineam istam
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 et perfice eam quam plantavit dextera tua et super filium quem confirmasti tibi
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 incensa igni et suffossa ab increpatione vultus tui peribunt
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 fiat manus tua super virum dexterae tuae et super filium hominis quem confirmasti tibi
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 et non discedimus a te vivificabis nos et nomen tuum invocabimus
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Domine Deus virtutum converte nos et ostende faciem tuam et salvi erimus
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.