< Psalmorum 78 >
1 intellectus Asaph adtendite populus meus legem meam inclinate aurem vestram in verba oris mei
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 aperiam in parabola os meum eloquar propositiones ab initio
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 quanta audivimus et cognovimus ea et patres nostri narraverunt nobis
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 non sunt occultata a filiis eorum in generationem alteram narrantes laudes Domini et virtutes eius et mirabilia eius quae fecit
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 et suscitavit testimonium in Iacob et legem posuit in Israhel quanta mandavit patribus nostris nota facere ea filiis suis
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 ut cognoscat generatio altera filii qui nascentur et exsurgent et narrabunt filiis suis
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 ut ponant in Deo spem suam et non obliviscantur opera Dei et mandata eius exquirant
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 ne fiant sicut patres eorum generatio prava et exasperans generatio quae non direxit cor suum et non est creditus cum Deo spiritus eius
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 filii Effrem intendentes et mittentes arcus conversi sunt in die belli
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 non custodierunt testamentum Dei et in lege eius noluerunt ambulare
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 et obliti sunt benefactorum eius et mirabilium eius quae ostendit eis
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 coram patribus eorum quae fecit mirabilia in terra Aegypti in campo Taneos
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 interrupit mare et perduxit eos statuit aquas quasi utrem
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 et deduxit eos in nube diei et tota nocte in inluminatione ignis
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 interrupit petram in heremo et adaquavit eos velut in abysso multa
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 et eduxit aquam de petra et deduxit tamquam flumina aquas
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 et adposuerunt adhuc peccare ei in ira excitaverunt Excelsum in inaquoso
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 et temptaverunt Deum in cordibus suis ut peterent escas animabus suis
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 et male locuti sunt de Deo dixerunt numquid poterit Deus parare mensam in deserto
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 quoniam percussit petram et fluxerunt aquae et torrentes inundaverunt numquid et panem potest dare aut parare mensam populo suo
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 ideo audivit Dominus et distulit et ignis accensus est in Iacob et ira ascendit in Israhel
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 quia non crediderunt in Deo nec speraverunt in salutare eius
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 et mandavit nubibus desuper et ianuas caeli aperuit
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 et pluit illis manna ad manducandum et panem caeli dedit eis
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 panem angelorum manducavit homo cibaria misit eis in abundantiam
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 transtulit austrum de caelo et induxit in virtute sua africum
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 et pluit super eos sicut pulverem carnes et sicut harenam maris volatilia pinnata
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 et ceciderunt in medio castrorum eorum circa tabernacula eorum
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 et manducaverunt et saturati sunt nimis et desiderium eorum adtulit eis
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 non sunt fraudati a desiderio suo adhuc escae eorum erant in ore ipsorum
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 et ira Dei ascendit in eos et occidit pingues eorum et electos Israhel inpedivit
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 in omnibus his peccaverunt adhuc et non crediderunt mirabilibus eius
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 et defecerunt in vanitate dies eorum et anni eorum cum festinatione
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 cum occideret eos quaerebant eum et revertebantur et diluculo veniebant ad Deum
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 et rememorati sunt quia Deus adiutor est eorum et Deus excelsus redemptor eorum est
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 et dilexerunt eum in ore suo et lingua sua mentiti sunt ei
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 cor autem ipsorum non erat rectum cum eo nec fideles habiti sunt in testamento eius
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 ipse autem est misericors et propitius fiet peccatis eorum et non perdet eos et abundabit ut avertat iram suam et non accendet omnem iram suam
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 et recordatus est quia caro sunt spiritus vadens et non rediens
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 quotiens exacerbaverunt eum in deserto in ira concitaverunt eum in inaquoso
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 et conversi sunt et temptaverunt Deum et Sanctum Israhel exacerbaverunt
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 non sunt recordati manus eius die qua redemit eos de manu tribulantis
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 sicut posuit in Aegypto signa sua et prodigia sua in campo Taneos
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 et convertit in sanguine flumina eorum et imbres eorum ne biberent
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 misit in eos cynomiam et comedit eos et ranam et disperdit eos
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 et dedit erugini fructus eorum et labores eorum lucustae
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 et occidit in grandine vineam eorum et moros eorum in pruina
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 et tradidit grandini iumenta eorum et possessionem eorum igni
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 misit in eos iram indignationis suae indignationem et iram et tribulationem inmissionem per angelos malos
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 viam fecit semitae irae suae non pepercit a morte animarum eorum et iumenta eorum in morte conclusit
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 et percussit omne primitivum in terra Aegypti primitias laborum eorum in tabernaculis Cham
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 et abstulit sicut oves populum suum et perduxit eos tamquam gregem in deserto
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 et deduxit eos in spe et non timuerunt et inimicos eorum operuit mare
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 et induxit eos in montem sanctificationis suae montem quem adquisivit dextera eius et eiecit a facie eorum gentes et sorte divisit eis terram in funiculo distributionis
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 et habitare fecit in tabernaculis eorum tribus Israhel
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 et temptaverunt et exacerbaverunt Deum excelsum et testimonia eius non custodierunt
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 et averterunt se et non servaverunt pactum quemadmodum patres eorum conversi sunt in arcum pravum
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 et in ira concitaverunt eum in collibus suis et in sculptilibus suis ad aemulationem eum provocaverunt
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 audivit Deus et sprevit et ad nihilum redegit valde Israhel
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 et reppulit tabernaculum Selo tabernaculum suum ubi habitavit in hominibus
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 et tradidit in captivitatem virtutem eorum et pulchritudinem eorum in manus inimici
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 et conclusit in gladio populum suum et hereditatem suam sprevit
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 iuvenes eorum comedit ignis et virgines eorum non sunt lamentatae
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 sacerdotes eorum in gladio ceciderunt et viduae eorum non plorabuntur
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 et excitatus est tamquam dormiens Dominus tamquam potens crapulatus a vino
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 et percussit inimicos suos in posteriora obprobrium sempiternum dedit illis
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 et reppulit tabernaculum Ioseph et tribum Effrem non elegit
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 et elegit tribum Iuda montem Sion quem dilexit
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 et aedificavit sicut unicornium sanctificium suum in terra quam fundavit in saecula
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 et elegit David servum suum et sustulit eum de gregibus ovium de post fetantes accepit eum
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 pascere Iacob servum suum et Israhel hereditatem suam
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 et pavit eos in innocentia cordis sui et in intellectibus manuum suarum deduxit eos
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.