< Psalmorum 77 >
1 in finem pro Idithun psalmus Asaph voce mea ad Dominum clamavi voce mea ad Deum et intendit me
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 in die tribulationis meae Deum exquisivi manibus meis nocte contra eum et non sum deceptus rennuit consolari anima mea
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 memor fui Dei et delectatus sum exercitatus sum et defecit spiritus meus diapsalma
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 anticipaverunt vigilias oculi mei turbatus sum et non sum locutus
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 cogitavi dies antiquos et annos aeternos in mente habui
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 et meditatus sum nocte cum corde meo exercitabar et scobebam spiritum meum
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 numquid in aeternum proiciet Deus et non adponet ut conplacitior sit adhuc
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 aut in finem misericordiam suam abscidet a generatione in generationem
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 aut obliviscetur misereri Deus aut continebit in ira sua misericordias suas diapsalma
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 et dixi nunc coepi haec mutatio dexterae Excelsi
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 memor fui operum Domini quia memor ero ab initio mirabilium tuorum
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 et meditabor in omnibus operibus tuis et in adinventionibus tuis exercebor
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Deus in sancto via tua quis deus magnus sicut Deus noster
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 tu es Deus qui facis mirabilia notam fecisti in populis virtutem tuam
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 redemisti in brachio tuo populum tuum filios Iacob et Ioseph diapsalma
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 viderunt te aquae Deus viderunt te aquae et timuerunt et turbatae sunt abyssi
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 multitudo sonitus aquarum vocem dederunt nubes etenim sagittae tuae transeunt
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 vox tonitrui tui in rota inluxerunt coruscationes tuae orbi terrae commota est et contremuit terra
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 in mari via tua et semitae tuae in aquis multis et vestigia tua non cognoscentur
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 deduxisti sicut oves populum tuum in manu Mosi et Aaron
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.