< Psalmorum 68 >

1 in finem David psalmus cantici exsurgat Deus et dissipentur inimici eius et fugiant qui oderunt eum a facie eius
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 sicut deficit fumus deficiant sicut fluit cera a facie ignis sic pereant peccatores a facie Dei
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 et iusti epulentur exultent in conspectu Dei delectentur in laetitia
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 cantate Deo psalmum dicite nomini eius iter facite ei qui ascendit super occasum Dominus nomen illi et exultate in conspectu eius turbabuntur a facie eius
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 patris orfanorum et iudicis viduarum Deus in loco sancto suo
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 Deus inhabitare facit unius moris in domo qui educit vinctos in fortitudine similiter eos qui exasperant qui habitant in sepulchris
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 Deus cum egredereris in conspectu populi tui cum pertransieris in deserto diapsalma
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 terra mota est etenim caeli distillaverunt a facie Dei Sinai a facie Dei Israhel
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 pluviam voluntariam segregabis Deus hereditati tuae et infirmata est tu vero perfecisti eam
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 animalia tua habitant in ea parasti in dulcedine tua pauperi Deus
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 Dominus dabit verbum evangelizantibus virtute multa
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 rex virtutum dilecti dilecti; et speciei domus dividere spolia
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 si dormiatis inter medios cleros pinnae columbae deargentatae et posteriora dorsi eius in pallore auri
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 dum discernit Caelestis reges super eam nive dealbabuntur in Selmon
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 mons Dei mons pinguis mons coagulatus mons pinguis
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 ut quid suspicamini montes coagulatos mons in quo beneplacitum est Deo habitare in eo etenim Dominus habitabit in finem
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 currus Dei decem milibus multiplex milia laetantium Dominus in eis in Sina in sancto
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 ascendisti in altum cepisti captivitatem accepisti dona in hominibus etenim non credentes inhabitare Dominum Deus
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 benedictus Dominus die cotidie prosperum iter faciet nobis Deus salutarium nostrorum diapsalma
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Deus noster Deus salvos faciendi et Domini Domini exitus mortis
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 verumtamen Deus confringet capita inimicorum suorum verticem capilli perambulantium in delictis suis
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 dixit Dominus ex Basan convertam convertam in profundis maris
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 ut intinguatur pes tuus in sanguine lingua canum tuorum ex inimicis ab ipso
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 viderunt ingressus tui Deus ingressus Dei mei regis mei qui est in sancto
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 praevenerunt principes coniuncti psallentibus in medio iuvencularum tympanistriarum
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 in ecclesiis benedicite Deum Dominum de fontibus Israhel
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 ibi Beniamin adulescentulus in mentis excessu principes Iuda duces eorum principes Zabulon principes Nepthali
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 manda Deus virtutem tuam confirma Deus hoc quod operatus es nobis
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 a templo tuo in Hierusalem tibi adferent reges munera
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 increpa feras harundinis congregatio taurorum in vaccis populorum ut excludant eos qui probati sunt argento dissipa gentes quae bella volunt
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 venient legati ex Aegypto Aethiopia praeveniet manus eius Deo
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 regna terrae cantate Deo psallite Domino diapsalma psallite Deo
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 qui ascendit super caelum caeli ad orientem ecce dabit voci suae vocem virtutis
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 date gloriam Deo super Israhel magnificentia eius et virtus eius in nubibus
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 mirabilis Deus in sanctis suis Deus Israhel ipse dabit virtutem et fortitudinem plebi suae benedictus Deus
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalmorum 68 >