< Psalmorum 6 >
1 in finem in carminibus pro octava psalmus David Domine ne in furore tuo arguas me neque in ira tua corripias me
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 miserere mei Domine quoniam infirmus sum sana me Domine quoniam conturbata sunt ossa mea
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 et anima mea turbata est valde et tu Domine usquequo
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 convertere Domine eripe animam meam salvum me fac propter misericordiam tuam
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 quoniam non est in morte qui memor sit tui in inferno autem quis confitebitur tibi (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 laboravi in gemitu meo lavabo per singulas noctes lectum meum in lacrimis meis stratum meum rigabo
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 turbatus est a furore oculus meus inveteravi inter omnes inimicos meos
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 discedite a me omnes qui operamini iniquitatem quoniam exaudivit Dominus vocem fletus mei
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 exaudivit Dominus deprecationem meam Dominus orationem meam suscepit
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 erubescant et conturbentur vehementer omnes inimici mei convertantur et erubescant valde velociter
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.