< Psalmorum 35 >

1 huic David iudica Domine nocentes me expugna expugnantes me
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami, upigane na hao wanaopigana nami.
2 adprehende arma et scutum et exsurge in adiutorium mihi
Chukua ngao na kigao. Inuka unisaidie.
3 effunde frameam et conclude adversus eos qui persequuntur me dic animae meae salus tua ego sum
Inua mkuki wako na fumo lako dhidi ya hao wanaonifuatia. Iambie nafsi yangu, “Mimi ni wokovu wako.”
4 confundantur et revereantur quaerentes animam meam avertantur retrorsum et confundantur cogitantes mihi mala
Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
5 fiant tamquam pulvis ante faciem venti et angelus Domini coartans eos
Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
6 fiat via illorum tenebrae et lubricum et angelus Domini persequens eos
Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
7 quoniam gratis absconderunt mihi interitum laquei sui supervacue exprobraverunt animam meam
Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
8 veniat illi laqueus quem ignorat et captio quam abscondit conprehendat eum et in laqueo cadat in ipso
maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
9 anima autem mea exultabit in Domino delectabitur super salutari suo
Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana na kuufurahia wokovu wake.
10 omnia ossa mea dicent Domine quis similis tui eripiens inopem de manu fortiorum eius egenum et pauperem a diripientibus eum
Nitapaza sauti yangu nikisema, “Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana? Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao, maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”
11 surgentes testes iniqui quae ignorabam interrogabant me
Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
12 retribuebant mihi mala pro bonis sterilitatem animae meae
Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
13 ego autem cum mihi molesti essent induebar cilicio humiliabam in ieiunio animam meam et oratio mea in sinum meum convertetur
Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,
14 quasi proximum quasi fratrem nostrum sic conplacebam quasi lugens et contristatus sic humiliabar
niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.
15 et adversum me laetati sunt et convenerunt congregata sunt super me flagella et ignoravi
Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.
16 dissipati sunt nec conpuncti temptaverunt me subsannaverunt me subsannatione frenduerunt super me dentibus suis
Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
17 Domine quando respicies restitue animam meam a malignitate eorum a leonibus unicam meam
Ee Bwana, utatazama mpaka lini? Niokoe maisha yangu na maangamizi yao, uhai wangu wa thamani kutokana na simba hawa.
18 confitebor tibi in ecclesia magna in populo gravi laudabo te
Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa, nitakusifu katikati ya watu wengi.
19 non supergaudeant mihi qui adversantur mihi inique qui oderunt me gratis et annuunt oculis
Usiwaache wale wanaonisimanga, wale ambao ni adui zangu bila sababu; usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu wakonyeze jicho kwa hila.
20 quoniam mihi quidem pacifice loquebantur et in iracundia terrae loquentes; dolos cogitabant
Hawazungumzi kwa amani, bali wanatunga mashtaka ya uongo dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.
21 et dilataverunt super me os suum dixerunt euge euge viderunt oculi nostri
Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”
22 vidisti Domine ne sileas Domine ne discedas a me
Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya. Usiwe mbali nami, Ee Bwana.
23 exsurge et intende iudicio meo Deus meus et Dominus meus in causam meam
Amka, inuka unitetee! Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.
24 iudica me secundum iustitiam tuam Domine Deus meus et non supergaudeant mihi
Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu, sawasawa na haki yako; usiwaache wakusimange.
25 non dicant in cordibus suis euge euge animae nostrae nec dicant devoravimus eum
Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!” Au waseme, “Tumemmeza.”
26 erubescant et revereantur simul qui gratulantur malis meis induantur confusione et reverentia qui magna loquuntur super me
Wote wanaofurahia dhiki yangu waaibishwe na wachanganyikiwe; hao wanaojiinua dhidi yangu wavikwe aibu na dharau.
27 exultent et laetentur qui volunt iustitiam meam et dicant semper magnificetur Dominus qui volunt pacem servi eius
Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki wapige kelele za shangwe na furaha; hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe, ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”
28 et lingua mea meditabitur iustitiam tuam tota die laudem tuam
Ulimi wangu utanena haki yako na sifa zako mchana kutwa.

< Psalmorum 35 >