< Psalmorum 33 >
1 psalmus David exultate iusti in Domino rectos decet laudatio
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 confitemini Domino in cithara in psalterio decem cordarum psallite illi
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 cantate ei canticum novum bene psallite in vociferatione
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 quia rectum est verbum Domini et omnia opera eius in fide
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 diligit misericordiam et iudicium misericordia Domini plena est terra
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 verbo Domini caeli firmati sunt et spiritu oris eius omnis virtus eorum
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 congregans sicut in utre aquas maris ponens in thesauris abyssos
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 timeat Dominum omnis terra ab eo autem commoveantur omnes inhabitantes orbem
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 quoniam ipse dixit et facta sunt ipse mandavit et creata sunt
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 Dominus dissipat consilia gentium reprobat autem cogitationes populorum et reprobat consilia principum
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 consilium autem Domini in aeternum manet cogitationes cordis eius in generatione et generationem
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 beata gens cuius est Dominus Deus eius populus quem elegit in hereditatem sibi
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 de caelo respexit Dominus vidit omnes filios hominum
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 de praeparato habitaculo suo respexit super omnes qui habitant terram
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 qui finxit singillatim corda eorum qui intellegit omnia opera illorum
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 non salvatur rex per multam virtutem et gigans non salvabitur in multitudine virtutis suae
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 fallax equus ad salutem in abundantia autem virtutis suae non salvabitur
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 ecce oculi Domini super metuentes eum qui sperant super misericordia eius
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 ut eruat a morte animas eorum et alat eos in fame
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 anima nostra sustinet Dominum quoniam adiutor et protector noster est
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 quia in eo laetabitur cor nostrum et in nomine sancto eius speravimus
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 fiat misericordia tua Domine super nos quemadmodum speravimus in te
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.