< Psalmorum 26 >
1 psalmus David iudica me Domine quoniam ego in innocentia mea ingressus sum et in Domino sperans non infirmabor
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 proba me Domine et tempta me ure renes meos et cor meum
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 quoniam misericordia tua ante oculos meos est et conplacui in veritate tua
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 non sedi cum concilio vanitatis et cum iniqua gerentibus non introibo
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 odivi ecclesiam malignantium et cum impiis non sedebo
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 lavabo inter innocentes manus meas et circumdabo altare tuum Domine
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 ut audiam vocem laudis et enarrem universa mirabilia tua
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Domine dilexi decorem domus tuae et locum habitationis gloriae tuae
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 ne perdas cum impiis animam meam et cum viris sanguinum vitam meam
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 in quorum manibus iniquitates sunt dextera eorum repleta est muneribus
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 ego autem in innocentia mea ingressus sum redime me et miserere mei
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 pes meus stetit in directo in ecclesiis benedicam te Domine
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.