< Psalmorum 19 >

1 in finem psalmus David caeli enarrant gloriam Dei et opera manuum eius adnuntiat firmamentum
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 dies diei eructat verbum et nox nocti indicat scientiam
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 non sunt loquellae neque sermones quorum non audiantur voces eorum
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4 in omnem terram exivit sonus eorum et in fines orbis terrae verba eorum
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 in sole posuit tabernaculum suum et ipse tamquam sponsus procedens de thalamo suo exultavit ut gigans ad currendam viam suam
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6 a summo caeli egressio eius et occursus eius usque ad summum eius nec est qui se abscondat a calore eius
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
7 lex Domini inmaculata convertens animas testimonium Domini fidele sapientiam praestans parvulis
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
8 iustitiae Domini rectae laetificantes corda praeceptum Domini lucidum inluminans oculos
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
9 timor Domini sanctus permanens in saeculum saeculi iudicia Domini vera iustificata in semet ipsa
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
10 desiderabilia super aurum et lapidem pretiosum multum et dulciora super mel et favum
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
11 etenim servus tuus custodit ea in custodiendis illis retributio multa
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12 delicta quis intellegit ab occultis meis munda me
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13 et ab alienis parce servo tuo si mei non fuerint dominati tunc inmaculatus ero et emundabor a delicto maximo
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
14 et erunt ut conplaceant eloquia oris mei et meditatio cordis mei in conspectu tuo semper Domine adiutor meus et redemptor meus
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.

< Psalmorum 19 >