< Psalmorum 132 >

1 canticum graduum memento Domine David et omnis mansuetudinis eius
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 sicut iuravit Domino votum vovit Deo Iacob
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 si introiero in tabernaculum domus meae si ascendero in lectum strati mei
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 si dedero somnum oculis meis et palpebris meis dormitationem
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 et requiem temporibus meis donec inveniam locum Domino tabernaculum Deo Iacob
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 ecce audivimus eam in Efrata invenimus eam in campis silvae
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 introibimus in tabernacula eius adorabimus in loco ubi steterunt pedes eius
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 surge Domine in requiem tuam tu et arca sanctificationis tuae
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 sacerdotes tui induentur iustitia et sancti tui exultabunt
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 propter David servum tuum non avertas faciem christi tui
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 iuravit Dominus David veritatem et non frustrabit eum de fructu ventris tui ponam super sedem tuam
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 si custodierint filii tui testamentum meum et testimonia mea haec quae docebo eos et filii eorum usque in saeculum sedebunt super sedem tuam
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 quoniam elegit Dominus Sion elegit eam in habitationem sibi
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 haec requies mea in saeculum saeculi hic habitabo quoniam elegi eam
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 viduam eius benedicens benedicam pauperes eius saturabo panibus
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 sacerdotes eius induam salutari et sancti eius exultatione exultabunt
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 illic producam cornu David paravi lucernam christo meo
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 inimicos eius induam confusione super ipsum autem efflorebit sanctificatio mea
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalmorum 132 >