< Psalmorum 124 >
1 canticum graduum huic David nisi quia Dominus erat in nobis dicat nunc Israhel
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2 nisi quia Dominus erat in nobis cum exsurgerent in nos homines
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
3 forte vivos degluttissent nos cum irasceretur furor eorum in nos
wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
4 forsitan aqua absorbuisset nos
mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
5 torrentem pertransivit anima nostra forsitan pertransisset anima nostra aquam intolerabilem
maji yaendayo kasi yangalituchukua.
6 benedictus Dominus qui non dedit nos in captionem dentibus eorum
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 anima nostra sicut passer erepta est de laqueo venantium laqueus contritus est et nos liberati sumus
Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
8 adiutorium nostrum in nomine Domini qui fecit caelum et terram
Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.