< Psalmorum 120 >
1 canticum graduum ad Dominum cum tribularer clamavi et exaudivit me
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Domine libera animam meam a labiis iniquis a lingua dolosa
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 quid detur tibi et quid adponatur tibi ad linguam dolosam
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 sagittae potentis acutae cum carbonibus desolatoriis
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 heu mihi quia incolatus meus prolongatus est habitavi cum habitationibus Cedar
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 multum incola fuit anima mea
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 cum his qui oderant pacem eram pacificus cum loquebar illis inpugnabant me gratis
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.