< Psalmorum 12 >

1 in finem pro octava psalmus David salvum me fac Domine quoniam defecit sanctus quoniam deminutae sunt veritates a filiis hominum
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2 vana locuti sunt unusquisque ad proximum suum labia dolosa in corde et corde locuti sunt
Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3 disperdat Dominus universa labia dolosa linguam magniloquam
Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
4 qui dixerunt linguam nostram magnificabimus labia nostra a nobis sunt quis noster dominus est
ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
5 propter miseriam inopum et gemitum pauperum nunc exsurgam dicit Dominus ponam in salutari fiducialiter agam in eo
“Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
6 eloquia Domini eloquia casta argentum igne examinatum probatum terrae purgatum septuplum
Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
7 tu Domine servabis nos et custodies nos a generatione hac et in aeternum
Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
8 in circuitu impii ambulant secundum altitudinem tuam multiplicasti filios hominum
Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

< Psalmorum 12 >