< Psalmorum 113 >
1 alleluia laudate pueri Dominum laudate nomen Domini
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 sit nomen Domini benedictum ex hoc nunc et usque in saeculum
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 a solis ortu usque ad occasum laudabile nomen Domini
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 excelsus super omnes gentes Dominus super caelos gloria eius
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 quis sicut Dominus Deus noster qui in altis habitat
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 et humilia respicit in caelo et in terra
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 suscitans a terra inopem et de stercore erigens pauperem
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 ut conlocet eum cum principibus cum principibus populi sui
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 qui habitare facit sterilem in domo matrem filiorum laetantem
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.