< Psalmorum 112 >
1 alleluia reversionis Aggei et Zacchariae beatus vir qui timet Dominum in mandatis eius volet nimis
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 potens in terra erit semen eius generatio rectorum benedicetur
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 gloria et divitiae in domo eius et iustitia eius manet in saeculum saeculi
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 exortum est in tenebris lumen rectis misericors et miserator et iustus
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 iucundus homo qui miseretur et commodat disponet sermones suos in iudicio
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 quia in aeternum non commovebitur
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 in memoria aeterna erit iustus ab auditione mala non timebit paratum cor eius sperare in Domino
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 confirmatum est cor eius non commovebitur donec dispiciat inimicos suos
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 dispersit dedit pauperibus iustitia eius manet in saeculum saeculi cornu eius exaltabitur in gloria
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 peccator videbit et irascetur dentibus suis fremet et tabescet desiderium peccatorum peribit
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.