< Proverbiorum 9 >
1 sapientia aedificavit sibi domum excidit columnas septem
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 immolavit victimas suas miscuit vinum et proposuit mensam suam
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 misit ancillas suas ut vocarent ad arcem et ad moenia civitatis
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 si quis est parvulus veniat ad me et insipientibus locuta est
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 venite comedite panem meum et bibite vinum quod miscui vobis
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 relinquite infantiam et vivite et ambulate per vias prudentiae
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 qui erudit derisorem ipse sibi facit iniuriam et qui arguit impium generat maculam sibi
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 noli arguere derisorem ne oderit te argue sapientem et diliget te
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 da sapienti et addetur ei sapientia doce iustum et festinabit accipere
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 principium sapientiae timor Domini et scientia sanctorum prudentia
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 per me enim multiplicabuntur dies tui et addentur tibi anni vitae
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 si sapiens fueris tibimet ipsi eris si inlusor solus portabis malum
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 mulier stulta et clamosa plenaque inlecebris et nihil omnino sciens
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 sedit in foribus domus suae super sellam in excelso urbis loco
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 ut vocaret transeuntes viam et pergentes itinere suo
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 quis est parvulus declinet ad me et vecordi locuta est
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 aquae furtivae dulciores sunt et panis absconditus suavior
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 et ignoravit quod gigantes ibi sint et in profundis inferni convivae eius (Sheol )
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )