< Proverbiorum 6 >
1 fili mi si spoponderis pro amico tuo defixisti apud extraneum manum tuam
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2 inlaqueatus es verbis oris tui et captus propriis sermonibus
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 fac ergo quod dico fili mi et temet ipsum libera quia incidisti in manu proximi tui discurre festina suscita amicum tuum
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
4 ne dederis somnum oculis tuis nec dormitent palpebrae tuae
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5 eruere quasi dammula de manu et quasi avis de insidiis aucupis
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
6 vade ad formicam o piger et considera vias eius et disce sapientiam
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
7 quae cum non habeat ducem nec praeceptorem nec principem
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
8 parat aestate cibum sibi et congregat in messe quod comedat
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 usquequo piger dormis quando consurges ex somno tuo
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
10 paululum dormies paululum dormitabis paululum conseres manus ut dormias
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11 et veniet tibi quasi viator egestas et pauperies quasi vir armatus
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
12 homo apostata vir inutilis graditur ore perverso
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
13 annuit oculis terit pede digito loquitur
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
14 pravo corde machinatur malum et in omni tempore iurgia seminat
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15 huic extemplo veniet perditio sua et subito conteretur nec habebit ultra medicinam
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16 sex sunt quae odit Dominus et septimum detestatur anima eius
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
17 oculos sublimes linguam mendacem manus effundentes innoxium sanguinem
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
18 cor machinans cogitationes pessimas pedes veloces ad currendum in malum
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
19 proferentem mendacia testem fallacem et eum qui seminat inter fratres discordias
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
20 conserva fili mi praecepta patris tui et ne dimittas legem matris tuae
Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 liga ea in corde tuo iugiter et circumda gutturi tuo
Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
22 cum ambulaveris gradiantur tecum cum dormieris custodiant te et evigilans loquere cum eis
Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
23 quia mandatum lucerna est et lex lux et via vitae increpatio disciplinae
Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
24 ut custodiant te a muliere mala et a blanda lingua extraneae
yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
25 non concupiscat pulchritudinem eius cor tuum nec capiaris nutibus illius
Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
26 pretium enim scorti vix unius est panis mulier autem viri pretiosam animam capit
kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
27 numquid abscondere potest homo ignem in sinu suo ut vestimenta illius non ardeant
Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
28 aut ambulare super prunas et non conburentur plantae eius
Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
29 sic qui ingreditur ad mulierem proximi sui non erit mundus cum tetigerit eam
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
30 non grandis est culpae cum quis furatus fuerit furatur enim ut esurientem impleat animam
Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
31 deprehensus quoque reddet septuplum et omnem substantiam domus suae tradet
Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
32 qui autem adulter est propter cordis inopiam perdet animam suam
Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 turpitudinem et ignominiam congregat sibi et obprobrium illius non delebitur
Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
34 quia zelus et furor viri non parcet in die vindictae
kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 nec adquiescet cuiusquam precibus nec suscipiet pro redemptione dona plurima
Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.