< Proverbiorum 3 >
1 fili mi ne obliviscaris legis meae et praecepta mea custodiat cor tuum
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 longitudinem enim dierum et annos vitae et pacem adponent tibi
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3 misericordia et veritas non te deserant circumda eas gutturi tuo et describe in tabulis cordis tui
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4 et invenies gratiam et disciplinam bonam coram Deo et hominibus
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5 habe fiduciam in Domino ex toto corde tuo et ne innitaris prudentiae tuae
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 in omnibus viis tuis cogita illum et ipse diriget gressus tuos
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7 ne sis sapiens apud temet ipsum time Dominum et recede a malo
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8 sanitas quippe erit umbilico tuo et inrigatio ossuum tuorum
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9 honora Dominum de tua substantia et de primitiis omnium frugum tuarum
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10 et implebuntur horrea tua saturitate et vino torcularia redundabunt
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11 disciplinam Domini fili mi ne abicias nec deficias cum ab eo corriperis
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12 quem enim diligit Dominus corripit et quasi pater in filio conplacet sibi
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13 beatus homo qui invenit sapientiam et qui affluit prudentia
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14 melior est adquisitio eius negotiatione argenti et auro primo fructus eius
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15 pretiosior est cunctis opibus et omnia quae desiderantur huic non valent conparari
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16 longitudo dierum in dextera eius in sinistra illius divitiae et gloria
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17 viae eius viae pulchrae et omnes semitae illius pacificae
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18 lignum vitae est his qui adprehenderint eam et qui tenuerit eam beatus
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19 Dominus sapientia fundavit terram stabilivit caelos prudentia
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20 sapientia illius eruperunt abyssi et nubes rore concrescunt
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21 fili mi ne effluant haec ab oculis tuis custodi legem atque consilium
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22 et erit vita animae tuae et gratia faucibus tuis
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23 tunc ambulabis fiducialiter in via tua et pes tuus non inpinget
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24 si dormieris non timebis quiesces et suavis erit somnus tuus
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25 ne paveas repentino terrore et inruentes tibi potentias impiorum
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26 Dominus enim erit in latere tuo et custodiet pedem tuum ne capiaris
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27 noli prohibere benefacere eum qui potest si vales et ipse benefac
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28 ne dicas amico tuo vade et revertere et cras dabo tibi cum statim possis dare
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29 ne moliaris amico tuo malum cum ille in te habeat fiduciam
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30 ne contendas adversus hominem frustra cum ipse tibi nihil mali fecerit
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31 ne aemuleris hominem iniustum nec imiteris vias eius
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32 quia abominatio Domini est omnis inlusor et cum simplicibus sermocinatio eius
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33 egestas a Domino in domo impii habitacula autem iustorum benedicentur
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34 inlusores ipse deludet et mansuetis dabit gratiam
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35 gloriam sapientes possidebunt stultorum exaltatio ignominia
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.