< Proverbiorum 22 >

1 melius est nomen bonum quam divitiae multae super argentum et aurum gratia bona
Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 dives et pauper obviaverunt sibi utriusque operator est Dominus
Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 callidus vidit malum et abscondit se innocens pertransiit et adflictus est damno
Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 finis modestiae timor Domini divitiae et gloria et vita
Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 arma et gladii in via perversi custos animae suae longe recedit ab eis
Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 proverbium est adulescens iuxta viam suam etiam cum senuerit non recedet ab ea
Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7 dives pauperibus imperat et qui accipit mutuum servus est fenerantis
Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8 qui seminat iniquitatem metet mala et virga irae suae consummabitur
Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9 qui pronus est ad misericordiam benedicetur de panibus enim suis dedit pauperi
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10 eice derisorem et exibit cum eo iurgium cessabuntque causae et contumeliae
Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11 qui diligit cordis munditiam propter gratiam labiorum suorum habebit amicum regem
Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12 oculi Domini custodiunt scientiam et subplantantur verba iniqui
Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13 dicit piger leo foris in medio platearum occidendus sum
Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14 fovea profunda os alienae cui iratus est Dominus incidet in eam
Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15 stultitia conligata est in corde pueri et virga disciplinae fugabit eam
Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16 qui calumniatur pauperem ut augeat divitias suas dabit ipse ditiori et egebit
Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17 inclina aurem tuam et audi verba sapientium adpone autem cor ad doctrinam meam
Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18 quae pulchra erit tibi cum servaveris eam in ventre tuo et redundabit in labiis tuis
maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19 ut sit in Domino fiducia tua unde et ostendi eam tibi hodie
Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20 ecce descripsi eam tibi tripliciter in cogitationibus et scientia
Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21 ut ostenderem tibi firmitatem et eloquia veritatis respondere ex his illi qui misit te
kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22 non facias violentiam pauperi quia pauper est neque conteras egenum in porta
Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23 quia Dominus iudicabit causam eius et configet eos qui confixerint animam eius
maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24 noli esse amicus homini iracundo neque ambules cum viro furioso
Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25 ne forte discas semitas eius et sumas scandalum animae tuae
au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
26 noli esse cum his qui defigunt manus suas et qui vades se offerunt pro debitis
Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
27 si enim non habes unde restituas quid causae est ut tollat operimentum de cubili tuo
Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
28 ne transgrediaris terminos antiquos quos posuerunt patres tui
Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
29 vidisti virum velocem in opere suo coram regibus stabit nec erit ante ignobiles
Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

< Proverbiorum 22 >