< Proverbiorum 2 >

1 fili mi si susceperis sermones meos et mandata mea absconderis penes te
Mwanangu, kama ukiyapokea maneno yangu na kuzitunza amri zangu,
2 ut audiat sapientiam auris tua inclina cor tuum ad noscendam prudentiam
usikilize hekima na utaelekeza moyo wako katika ufahamu.
3 si enim sapientiam invocaveris et inclinaveris cor tuum prudentiae
kama utalilia ufahamu na kupaza sauti yako kwa ajili ya ufahamu,
4 si quaesieris eam quasi pecuniam et sicut thesauros effoderis illam
kama utautafuta kama fedha na kupekua ufahamu kama unatafuta hazina iliyojificha,
5 tunc intelleges timorem Domini et scientiam Dei invenies
ndipo utakapofahamu hofu ya Yehova na utapata maarifa ya Mungu.
6 quia Dominus dat sapientiam et ex ore eius scientia et prudentia
Kwa kuwa Yohova hutoa hekima, katika kinywa chake hutoka maarifa na ufahamu.
7 custodiet rectorum salutem et proteget gradientes simpliciter
Yeye huhifadhi sauti ya hekima kwa wale wampendezao, yeye ni ngao kwa wale waendao katika uadilifu,
8 servans semitas iustitiae et vias sanctorum custodiens
huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
9 tunc intelleges iustitiam et iudicium et aequitatem et omnem semitam bonam
Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
10 si intraverit sapientia cor tuum et scientia animae tuae placuerit
Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11 consilium custodiet te prudentia servabit te
Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12 ut eruaris de via mala ab homine qui perversa loquitur
Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13 qui relinquunt iter rectum et ambulant per vias tenebrosas
Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
14 qui laetantur cum malefecerint et exultant in rebus pessimis
Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
15 quorum viae perversae et infames gressus eorum
Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.
16 ut eruaris a muliere aliena et ab extranea quae mollit sermones suos
Busara na hekima zitakuokoa kutoka kwa mwanamke malaya, kutoka kwa mwanamke anayetafuta visa na mwenye maneno ya kubembeleza.
17 et relinquit ducem pubertatis suae
Yeye humwacha mwenzi wa ujana wake na kusahau agano la Mungu wake.
18 et pacti Dei sui oblita est inclinata est enim ad mortem domus eius et ad impios semitae ipsius
Maana nyumba yake huinama na kufa na mapito yake yatakupeleka kwa wale walioko kaburini.
19 omnes qui ingrediuntur ad eam non revertentur nec adprehendent semitas vitae
Wote waiendeao njia yake hawatarudi tena na wala hawataziona njia za uzima.
20 ut ambules in via bona et calles iustorum custodias
kwa hiyo utatembea katika njia ya watu wema na kufuata njia za wale watendao mema.
21 qui enim recti sunt habitabunt in terra et simplices permanebunt in ea
Kwa wale watendao mema watafanya makazi yao katika nchi, na wale wenye uadilifu watadumu katika nchi.
22 impii vero de terra perdentur et qui inique agunt auferentur ex ea
Lakini waovu wataondolewa katika nchi na wale wasioamini wataondolewa katika nchi.

< Proverbiorum 2 >