< Proverbiorum 18 >
1 occasiones quaerit qui vult recedere ab amico omni tempore erit exprobrabilis
Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
2 non recipit stultus verba prudentiae nisi ea dixeris quae versantur in corde eius
Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
3 impius cum in profundum venerit peccatorum contemnit sed sequitur eum ignominia et obprobrium
Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
4 aqua profunda verba ex ore viri et torrens redundans fons sapientiae
Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
5 accipere personam impii non est bonum ut declines a veritate iudicii
Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
6 labia stulti inmiscunt se rixis et os eius iurgia provocat
Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
7 os stulti contritio eius et labia illius ruina animae eius
Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
8 verba bilinguis quasi simplicia et ipsa perveniunt usque ad interiora ventris
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
9 qui mollis et dissolutus est in opere suo frater est sua opera dissipantis
Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10 turris fortissima nomen Domini ad ipsum currit iustus et exaltabitur
Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11 substantia divitis urbs roboris eius et quasi murus validus circumdans eum
Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12 antequam conteratur exaltatur cor hominis et antequam glorificetur humiliatur
Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
13 qui prius respondit quam audiat stultum se esse demonstrat et confusione dignum
Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
14 spiritus viri sustentat inbecillitatem suam spiritum vero ad irascendum facilem quis poterit sustinere
Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
15 cor prudens possidebit scientiam et auris sapientium quaerit doctrinam
Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
16 donum hominis dilatat viam eius et ante principes spatium ei facit
Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
17 iustus prior est accusator sui venit amicus eius et investigavit eum
Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
18 contradictiones conprimit sors et inter potentes quoque diiudicat
Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
19 frater qui adiuvatur a fratre quasi civitas firma et iudicia quasi vectes urbium
Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
20 de fructu oris viri replebitur venter eius et genimina labiorum illius saturabunt eum
Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
21 mors et vita in manu linguae qui diligunt eam comedent fructus eius
Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
22 qui invenit mulierem invenit bonum et hauriet iucunditatem a Domino
Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
23 cum obsecrationibus loquetur pauper et dives effabitur rigide
Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
24 vir amicalis ad societatem magis amicus erit quam frater
Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.