< Liber Numeri 2 >

1 locutusque est Dominus ad Mosen et Aaron dicens
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
2 singuli per turmas signa atque vexilla et domos cognationum suarum castrametabuntur filiorum Israhel per gyrum tabernaculi foederis
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
3 ad orientem Iudas figet tentoria per turmas exercitus sui eritque princeps filiorum eius Naasson filius Aminadab
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
4 et omnis de stirpe eius summa pugnantium septuaginta quattuor milia sescentorum
Kundi lake lina watu 74,600.
5 iuxta eum castrametati sunt de tribu Isachar quorum princeps fuit Nathanahel filius Suar
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
6 et omnis numerus pugnatorum eius quinquaginta quattuor milia quadringenti
Kundi lake lina watu 54,400.
7 in tribu Zabulon princeps fuit Heliab filius Helon
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
8 omnis de stirpe eius exercitus pugnatorum quinquaginta septem milia quadringenti
Kundi lake lina watu 57,400.
9 universi qui in castris Iudae adnumerati sunt fuerunt centum octoginta sex milia quadringenti et per turmas suas primi egredientur
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
10 in castris filiorum Ruben ad meridianam plagam erit princeps Elisur filius Sedeur
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
11 et cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt quadraginta sex milia quingenti
Kundi lake lina watu 46,500.
12 iuxta eum castrametati sunt de tribu Symeon quorum princeps fuit Salamihel filius Surisaddai
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
13 et cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt quinquaginta novem milia trecenti
Kundi lake lina watu 59,300.
14 in tribu Gad princeps fuit Heliasaph filius Duhel
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
15 et cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt quadraginta quinque milia sescenti quinquaginta
Kundi lake lina watu 45,650.
16 omnes qui recensiti sunt in castris Ruben centum quinquaginta milia et mille quadringenti quinquaginta per turmas suas in secundo loco proficiscentur
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
17 levabitur autem tabernaculum testimonii per officia Levitarum et turmas eorum quomodo erigetur ita et deponetur singuli per loca et ordines suos proficiscentur
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
18 ad occidentalem plagam erunt castra filiorum Ephraim quorum princeps fuit Helisama filius Ammiud
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt quadraginta milia quingenti
Kundi lake lina watu 40,500.
20 et cum eis tribus filiorum Manasse quorum princeps fuit Gamalihel filius Phadassur
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
21 cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt triginta duo milia ducenti
Kundi lake lina watu 32,200.
22 in tribu filiorum Beniamin princeps fuit Abidan filius Gedeonis
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
23 et cunctus exercitus pugnatorum eius qui recensiti sunt triginta quinque milia quadringenti
Kundi lake lina watu 35,400.
24 omnes qui numerati sunt in castris Ephraim centum octo milia centum per turmas suas tertii proficiscentur
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
25 ad aquilonis partem castrametati sunt filii Dan quorum princeps fuit Ahiezer filius Amisaddai
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt sexaginta duo milia septingenti
Kundi lake lina watu 62,700.
27 iuxta eum fixere tentoria de tribu Aser quorum princeps fuit Phegihel filius Ochran
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
28 cunctus exercitus pugnatorum eius qui numerati sunt quadraginta milia et mille quingenti
Kundi lake lina watu 41,500.
29 de tribu filiorum Nepthalim princeps fuit Ahira filius Henan
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 cunctus exercitus pugnatorum eius quinquaginta tria milia quadringenti
Kundi lake lina watu 53,400.
31 omnes qui numerati sunt in castris Dan fuerunt centum quinquaginta septem milia sescenti et novissimi proficiscentur
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
32 hic numerus filiorum Israhel per domos cognationum suarum et turmas divisi exercitus sescenta tria milia quingenti quinquaginta
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
33 Levitae autem non sunt numerati inter filios Israhel sic enim praecepit Dominus Mosi
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
34 feceruntque filii Israhel iuxta omnia quae mandaverat Dominus castrametati sunt per turmas suas et profecti per familias ac domos patrum suorum
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.

< Liber Numeri 2 >