< Nehemiæ 7 >

1 postquam autem aedificatus est murus et posui valvas et recensui ianitores et cantores et Levitas
Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2 praecepi Aneni fratri meo et Ananiae principi domus de Hierusalem ipse enim quasi vir verax et timens Deum plus ceteris videbatur
Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3 et dixi eis non aperiantur portae Hierusalem usque ad calorem solis cumque adhuc adsisterent clausae portae sunt et oppilatae et posui custodes de habitatoribus Hierusalem singulos per vices suas et unumquemque contra domum suam
Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
4 civitas autem erat lata nimis et grandis et populus parvus in medio eius et non erant domus aedificatae
Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5 dedit autem Deus in corde meo et congregavi optimates et magistratus et vulgum ut recenserem eos et inveni librum census eorum qui ascenderant primum et inventum est scriptum in eo
Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6 isti filii provinciae qui ascenderunt de captivitate migrantium quos transtulerat Nabuchodonosor rex Babylonis et reversi sunt in Hierusalem et in Iudaeam unusquisque in civitatem suam
Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7 qui venerunt cum Zorobabel Hiesuae Neemias Azarias Raamias Naamni Mardocheus Belsar Mespharath Beggoai Naum Baana numerus virorum populi Israhel
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8 filii Pharos duo milia centum septuaginta duo
wazao wa Paroshi 2,172
9 filii Saphatiae trecenti septuaginta duo
wazao wa Shefatia 372
10 filii Area sescenti quinquaginta duo
wazao wa Ara 652
11 filii Phaethmoab filiorum Hiesuae et Ioab duo milia octingenti decem et octo
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
12 filii Helam mille octingenti quinquaginta quattuor
wazao wa Elamu 1,254
13 filii Zethua octingenti quadraginta quinque
wazao wa Zatu 845
14 filii Zacchai septingenti sexaginta
wazao wa Zakai 760
15 filii Bennui sescenti quadraginta octo
wazao wa Binui 648
16 filii Bebai sescenti viginti octo
wazao wa Bebai 628
17 filii Azgad duo milia trecenti viginti duo
wazao wa Azgadi 2,322
18 filii Adonicam sescenti sexaginta septem
wazao wa Adonikamu 667
19 filii Baggoaim duo milia sexaginta septem
wazao wa Bigwai 2,067
20 filii Adin sescenti quinquaginta quinque
wazao wa Adini 655
21 filii Ater filii Ezechiae nonaginta octo
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 filii Asem trecenti viginti octo
wazao wa Hashumu 328
23 filii Besai trecenti viginti quattuor
wazao wa Besai 324
24 filii Areph centum duodecim
wazao wa Harifu 112
25 filii Gabaon nonaginta quinque
wazao wa Gibeoni 95
26 viri Bethleem et Netupha centum octoginta octo
watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 viri Anathoth centum viginti octo
watu wa Anathothi 128
28 viri Bethamoth quadraginta duo
watu wa Beth-Azmawethi 42
29 viri Cariathiarim Cephira et Beroth septingenti quadraginta tres
watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 viri Rama et Geba sescenti viginti unus
watu wa Rama na Geba 621
31 viri Machmas centum viginti duo
watu wa Mikmashi 122
32 viri Bethel et Hai centum viginti tres
watu wa Betheli na Ai 123
33 viri Nebo alterius quinquaginta duo
watu wa Nebo 52
34 viri Helam alterius mille ducenti quinquaginta quattuor
wazao wa Elamu 1,254
35 filii Arem trecenti viginti
wazao wa Harimu 320
36 filii Hiericho trecenti quadraginta quinque
wazao wa Yeriko 345
37 filii Lod Adid et Ono septingenti viginti unus
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 filii Senaa tria milia nongenti triginta
wazao wa Senaa 3,930
39 sacerdotes filii Idaia in domo Iosua nongenti septuaginta tres
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
40 filii Emmer mille quinquaginta duo
wazao wa Imeri 1,052
41 filii Phassur mille ducenti quadraginta septem
wazao wa Pashuri 1,247
42 filii Arem mille decem et septem Levitae
wazao wa Harimu 1,017
43 filii Iosue et Cadmihel filiorum
Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
44 Oduia septuaginta quattuor cantores
Waimbaji: wazao wa Asafu 148
45 filii Asaph centum quadraginta octo
Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
46 ianitores filii Sellum filii Ater filii Telmon filii Accub filii Atita filii Sobai centum triginta octo
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47 Nathinnei filii Soa filii Asfa filii Tebaoth
wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48 filii Ceros filii Siaa filii Fado filii Lebana filii Agaba filii Selmon
wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49 filii Anan filii Geddel filii Gaer
wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50 filii Raaia filii Rasim filii Necoda
wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51 filii Gezem filii Aza filii Fasea
wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52 filii Besai filii Munim filii Nephusim
wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53 filii Becbuc filii Acupha filii Arur
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54 filii Besloth filii Meida filii Arsa
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55 filii Bercos filii Sisara filii Thema
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56 filii Nesia filii Atipha
wazao wa Nesia na Hatifa.
57 filii servorum Salomonis filii Sotai filii Sophereth filii Pherida
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58 filii Iahala filii Dercon filii Geddel
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59 filii Saphatia filii Athil filii Phocereth qui erat ortus ex Sabaim filio Amon
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60 omnes Nathinnei et filii servorum Salomonis trecenti nonaginta duo
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
61 hii sunt autem qui ascenderunt de Thelmella Thelarsa Cherub Addon et Emmer et non potuerunt indicare domum patrum suorum et semen suum utrum ex Israhel essent
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
62 filii Dalaia filii Tobia filii Necoda sescenti quadraginta duo
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
63 et de sacerdotibus filii Abia filii Accos filii Berzellai qui accepit de filiabus Berzellai Galaditis uxorem et vocatus est nomine eorum
Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64 hii quaesierunt scripturam suam in censu et non invenerunt et eiecti sunt de sacerdotio
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65 dixitque Athersatha eis ut non manducarent de sanctis sanctorum donec staret sacerdos doctus et eruditus
Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
66 omnis multitudo quasi unus quadraginta duo milia sescenti sexaginta
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67 absque servis et ancillis eorum qui erant septem milia trecenti triginta et septem et inter eos cantores et cantrices ducentae quadraginta quinque
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69 cameli quadringenti triginta quinque asini sex milia septingenti viginti
ngamia 435 na punda 6,720.
70 nonnulli autem de principibus familiarum dederunt in opus Athersatha dedit in thesaurum auri dragmas mille fialas quinquaginta tunicas sacerdotales quingentas triginta
Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71 et de principibus familiarum dederunt in thesaurum operis auri dragmas viginti milia et argenti minas duo milia ducentas
Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72 et quod dedit reliquus populus auri dragmas viginti milia et argenti minas duo milia et tunicas sacerdotales sexaginta septem
Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73 habitaverunt autem sacerdotes et Levitae et ianitores et cantores et reliquum vulgus et Nathinnei et omnis Israhel in civitatibus suis
Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,

< Nehemiæ 7 >