< Nehemiæ 10 >

1 signatores autem fuerunt Neemias Athersatha filius Achelai et Sedecias
Wale waliotia muhuri walikuwa: Nehemia mtawala, mwana wa Hakalia. Sedekia,
2 Saraias Azarias Hieremias
Seraya, Azaria, Yeremia,
3 Phessur Amaria Melchia
Pashuri, Amaria, Malkiya,
4 Attus Sebenia Melluc
Hatushi, Shebania, Maluki,
5 Arem Mermuth Obdias
Harimu, Meremothi, Obadia,
6 Danihel Genton Baruch
Danieli, Ginethoni, Baruku,
7 Mosollam Abia Miamin
Meshulamu, Abiya, Miyamini,
8 Mazia Belga Semaia hii sacerdotes
Maazia, Bilgai na Shemaya. Hawa ndio waliokuwa makuhani.
9 porro Levitae Iosue filius Azaniae Bennui de filiis Enadad Cedmihel
Walawi: Yeshua mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli,
10 et fratres eorum Sechenia Odevia Celita Phalaia Anan
na wenzao: Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani,
11 Micha Roob Asebia
Mika, Rehobu, Hashabia,
12 Zacchur Serebia Sabania
Zakuri, Sherebia, Shebania,
13 Odia Bani Baninu
Hodia, Bani na Beninu.
14 capita populi Pheros Phaethmoab Helam Zethu Bani
Viongozi wa watu: Paroshi, Pahath-Moabu, Elamu, Zatu, Bani,
15 Bonni Azgad Bebai
Buni, Azgadi, Bebai,
16 Adonia Beggoai Adin
Adoniya, Bigwai, Adini,
17 Ater Ezechia Azur
Ateri, Hezekia, Azuri,
18 Odevia Asum Besai
Hodia, Hashumu, Besai,
19 Ares Anathoth Nebai
Harifu, Anathothi, Nebai,
20 Mecphia Mosollam Azir
Magpiashi, Meshulamu, Heziri,
21 Mesizabel Sadoc Ieddua
Meshezabeli, Sadoki, Yadua,
22 Felthia Anan Ania
Pelatia, Hanani, Anaya,
23 Osee Anania Asub
Hoshea, Hanania, Hashubu,
24 Aloes Phaleam Sobec
Haloheshi, Pilha, Shobeki,
25 Reum Asebna Madsia
Rehumu, Hashabna, Maaseya,
26 et Haia Hanam Anan
Ahiya, Hanani, Anani,
27 Melluc Arem Baana
Maluki, Harimu na Baana.
28 et reliqui de populo sacerdotes Levitae ianitores et cantores Nathinnei et omnes qui se separaverunt de populis terrarum ad legem Dei uxores eorum filii eorum et filiae eorum
“Watu wengine wote, wakiwa ni makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji, watumishi wa Hekalu, na wale wote waliojitenga na mataifa jirani kwa ajili ya Sheria ya Mungu, pamoja na wake zao na wana wao na binti zao wote waliokuwa na uwezo wa kufahamu,
29 omnis qui poterat sapere spondentes pro fratribus suis optimates eorum et qui veniebant ad pollicendum et iurandum ut ambularent in lege Dei quam dederat in manu Mosi servi Dei ut facerent et custodirent universa mandata Domini Dei nostri et iudicia eius et caerimonias eius
basi hawa wote wanajiunga na ndugu zao na wakuu wao, na kujifunga kwa laana na kwa kiapo kufuata Sheria ya Mungu iliyotolewa kupitia kwa Mose mtumishi wa Mungu, na kutii kwa uangalifu amri zote, maagizo na sheria za Bwana, Bwana wetu.
30 et ut non daremus filias nostras populo terrae et filias eorum non acciperemus filiis nostris
“Tunaahidi kutowaoza binti zetu kwa watu wanaotuzunguka, wala kuwaoza wana wetu binti zao.
31 populi quoque terrae qui inportant venalia et omnia ad usum per diem sabbati ut vendant non accipiemus ab eis in sabbato et in die sanctificata et dimittemus annum septimum et exactionem universae manus
“Wakati mataifa jirani waletapo bidhaa zao au nafaka kuuza siku ya Sabato, hatutazinunua kutoka kwao siku ya Sabato, wala siku nyingine yoyote takatifu. Kila mwaka wa saba, tutaacha kuilima ardhi na tutafuta madeni yote.
32 et statuemus super nos praecepta ut demus tertiam partem sicli per annum ad opus domus Dei nostri
“Tunakubali wajibu wa kutimiza amri za kutoa theluthi ya shekeli kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu:
33 ad panes propositionis et ad sacrificium sempiternum et in holocaustum sempiternum in sabbatis in kalendis in sollemnitatibus et in sanctificatis et pro peccato ut exoretur pro Israhel et in omnem usum domus Dei nostri
Kwa ajili ya mikate ya Wonyesho, kwa ajili ya sadaka za kawaida za nafaka na sadaka za kuteketezwa, kwa ajili ya sadaka za siku za Sabato, Sikukuu za Mwandamo wa Mwezi na sikukuu nyingine zilizoamriwa, kwa ajili ya sadaka takatifu, kwa ajili ya sadaka za dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu.
34 sortes ergo misimus super oblatione lignorum inter sacerdotes et Levitas et populos ut inferrentur in domum Dei nostri per domos patrum nostrorum per tempora a temporibus anni usque ad annum ut arderent super altare Domini Dei nostri sicut scriptum est in lege Mosi
“Sisi makuhani, Walawi na watu, tumepiga kura kuamua kuwa kila mmoja wa jamaa zetu lazima alete katika nyumba ya Mungu wetu kwa nyakati maalum kila mwaka mchango wa kuni za kukokea moto katika madhabahu ya Bwana Mungu wetu, kama ilivyoandikwa katika Sheria.
35 et ut adferremus primogenita terrae nostrae et primitiva universi fructus omnis ligni ab anno in annum in domo Domini
“Pia tunachukua wajibu wa kuleta malimbuko ya mazao yetu na matunda ya kwanza ya kila mti wa matunda katika nyumba ya Bwana kila mwaka.
36 et primitiva filiorum nostrorum et pecorum nostrorum sicut scriptum est in lege et primitiva boum nostrorum et ovium nostrarum ut offerrentur in domo Dei nostri sacerdotibus qui ministrant in domo Dei nostri
“Kama pia ilivyoandikwa katika Sheria, tutawaleta wazaliwa wetu wa kwanza wa kiume, na wa mifugo yetu, yaani wa ngʼombe wetu na wa makundi yetu ya kondoo na mbuzi, katika nyumba ya Mungu wetu, kwa ajili ya makuhani wanaohudumu huko.
37 et primitias ciborum nostrorum et libaminum nostrorum et poma omnis ligni vindemiae quoque et olei adferemus sacerdotibus ad gazofilacium Dei nostri et decimam partem terrae nostrae Levitis ipsi Levitae decimas accipient ex omnibus civitatibus operum nostrorum
“Zaidi ya hayo, tutaleta katika ghala za nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani, vyakula vya kwanza vya mashamba yetu, sadaka zetu za nafaka, matunda ya miti yetu yote, divai yetu mpya na mafuta. Nasi tutaleta zaka za mazao yetu kwa Walawi, kwa kuwa Walawi ndio ambao hukusanya zaka katika miji yote tunakofanya kazi.
38 erit autem sacerdos filius Aaron cum Levitis in decimis Levitarum et Levitae offerent decimam partem decimae suae in domum Dei nostri ad gazofilacium in domo thesauri
Kuhani atokanaye na uzao wa Aroni atashirikiana na Walawi wakati wanapopokea zaka, nao Walawi itawapasa kuleta sehemu ya kumi ya zaka katika nyumba ya Mungu wetu katika ghala za hazina.
39 ad gazofilacium enim deportabunt filii Israhel et filii Levi primitias frumenti vini et olei et ibi erunt vasa sanctificata et sacerdotes et cantores et ianitores et ministri et non dimittemus domum Dei nostri
Watu wa Israeli pamoja na Walawi itawapasa kuleta michango yao ya nafaka, divai mpya na mafuta katika vyumba vya ghala, mahali vifaa vya mahali patakatifu vinapohifadhiwa, na wanapokaa makuhani wanaohudumu, na mabawabu na waimbaji. “Hatutaacha kuijali nyumba ya Mungu wetu.”

< Nehemiæ 10 >