< Iosue 12 >
1 hii sunt reges quos percusserunt filii Israhel et possederunt terram eorum trans Iordanem ad solis ortum a torrente Arnon usque ad montem Hermon et omnem orientalem plagam quae respicit solitudinem
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Seon rex Amorreorum qui habitavit in Esebon dominatus est ab Aroer quae sita est super ripam torrentis Arnon et mediae partis in valle dimidiique Galaad usque ad torrentem Iaboc qui est terminus filiorum Ammon
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 et a solitudine usque ad mare Cheneroth contra orientem et usque ad mare Deserti quod est mare Salsissimum ad orientalem plagam per viam quae ducit Bethesimoth et ab australi parte quae subiacent Asedothphasga
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 terminus Og regis Basan de reliquiis Rafaim qui habitavit in Astharoth et in Edrain et dominatus est in monte Hermon et in Salacha atque in universa Basan usque ad terminos
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 Gesuri et Machathi et dimidiae partis Galaad terminos Seon regis Esebon
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moses famulus Domini et filii Israhel percusserunt eos tradiditque terram eorum Moses in possessionem Rubenitis et Gadditis et dimidiae tribui Manasse
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 hii sunt reges terrae quos percussit Iosue et filii Israhel trans Iordanem ad occidentalem plagam a Baalgad in campo Libani usque ad montem cuius pars ascendit in Seir tradiditque eam Iosue in possessionem tribubus Israhel singulis partes suas
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 tam in montanis quam in planis atque campestribus in Aseroth et solitudine ac meridie Hettheus fuit et Amorreus Chananeus et Ferezeus Eveus et Iebuseus
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 rex Hiericho unus rex Ahi quae est ex latere Bethel unus
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 rex Hierusalem unus rex Hebron unus
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 rex Hierimoth unus rex Lachis unus
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 rex Eglon unus rex Gazer unus
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 rex Dabir unus rex Gader unus
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 rex Herma unus rex Hered unus
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 rex Lebna unus rex Odollam unus
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 rex Maceda unus rex Bethel unus
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 rex Thaffua unus rex Afer unus
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 rex Afec unus rex Saron unus
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 rex Madon unus rex Asor unus
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 rex Someron unus rex Acsaph unus
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 rex Thenach unus rex Mageddo unus
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 rex Cades unus rex Iachanaem Chermeli unus
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 rex Dor et provinciae Dor unus rex gentium Galgal unus
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 rex Thersa unus omnes reges triginta et unus
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.