< Job 39 >

1 numquid nosti tempus partus hibicum in petris vel parturientes cervas observasti
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 dinumerasti menses conceptus earum et scisti tempus partus earum
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 incurvantur ad fetum et pariunt et rugitus emittunt
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 separantur filii earum pergunt ad pastum egrediuntur et non revertuntur ad eas
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 quis dimisit onagrum liberum et vincula eius quis solvit
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 cui dedi in solitudine domum et tabernacula eius in terra salsuginis
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 contemnit multitudinem civitatis clamorem exactoris non audit
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 circumspicit montes pascuae suae et virentia quaeque perquirit
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 numquid volet rinoceros servire tibi aut morabitur ad praesepe tuum
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 numquid alligabis rinocerota ad arandum loro tuo aut confringet glebas vallium post te
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 numquid fiduciam habebis in magna fortitudine eius et derelinques ei labores tuos
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 numquid credes ei quoniam reddat sementem tibi et aream tuam congreget
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 pinna strutionum similis est pinnis herodii et accipitris
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 quando derelinquit in terra ova sua tu forsitan in pulvere calefacis ea
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 obliviscitur quod pes conculcet ea aut bestiae agri conterant
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 duratur ad filios suos quasi non sint sui frustra laboravit nullo timore cogente
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 privavit enim eam Deus sapientia nec dedit illi intellegentiam
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 cum tempus fuerit in altum alas erigit deridet equitem et ascensorem eius
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 numquid praebebis equo fortitudinem aut circumdabis collo eius hinnitum
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 numquid suscitabis eum quasi lucustas gloria narium eius terror
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 terram ungula fodit exultat audacter in occursum pergit armatis
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 contemnit pavorem nec cedit gladio
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 super ipsum sonabit faretra vibrabit hasta et clypeus
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 fervens et fremens sorbet terram nec reputat tubae sonare clangorem
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 ubi audierit bucinam dicet va procul odoratur bellum exhortationem ducum et ululatum exercitus
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 numquid per sapientiam tuam plumescit accipiter expandens alas suas ad austrum
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 aut ad praeceptum tuum elevabitur aquila et in arduis ponet nidum suum
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 in petris manet et in praeruptis silicibus commoratur atque inaccessis rupibus
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 inde contemplatur escam et de longe oculi eius prospiciunt
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 pulli eius lambent sanguinem et ubicumque cadaver fuerit statim adest
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Job 39 >