< Job 38 >

1 respondens autem Dominus Iob de turbine dixit
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 quis est iste involvens sententias sermonibus inperitis
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 accinge sicut vir lumbos tuos interrogabo te et responde mihi
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 ubi eras quando ponebam fundamenta terrae indica mihi si habes intellegentiam
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 quis posuit mensuras eius si nosti vel quis tetendit super eam lineam
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 super quo bases illius solidatae sunt aut quis dimisit lapidem angularem eius
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 cum me laudarent simul astra matutina et iubilarent omnes filii Dei
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 quis conclusit ostiis mare quando erumpebat quasi de vulva procedens
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 cum ponerem nubem vestimentum eius et caligine illud quasi pannis infantiae obvolverem
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 circumdedi illud terminis meis et posui vectem et ostia
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 et dixi usque huc venies et non procedes amplius et hic confringes tumentes fluctus tuos
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 numquid post ortum tuum praecepisti diluculo et ostendisti aurorae locum suum
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 et tenuisti concutiens extrema terrae et excussisti impios ex ea
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 restituetur ut lutum signaculum et stabit sicut vestimentum
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 auferetur ab impiis lux sua et brachium excelsum confringetur
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 numquid ingressus es profunda maris et in novissimis abyssis deambulasti
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 numquid apertae tibi sunt portae mortis et ostia tenebrosa vidisti
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 numquid considerasti latitudines terrae indica mihi si nosti omnia
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 in qua via habitet lux et tenebrarum quis locus sit
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 ut ducas unumquodque ad terminos suos et intellegas semitas domus eius
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 sciebas tunc quod nasciturus esses et numerum dierum tuorum noveras
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 numquid ingressus es thesauros nivis aut thesauros grandinis aspexisti
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 quae praeparavi in tempus hostis in diem pugnae et belli
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 per quam viam spargitur lux dividitur aestus super terram
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 quis dedit vehementissimo imbri cursum et viam sonantis tonitrui
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 ut plueret super terram absque homine in deserto ubi nullus mortalium commoratur
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 ut impleret inviam et desolatam et produceret herbas virentes
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 quis est pluviae pater vel quis genuit stillas roris
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 de cuius utero egressa est glacies et gelu de caelo quis genuit
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 in similitudinem lapidis aquae durantur et superficies abyssi constringitur
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 numquid coniungere valebis micantes stellas Pliadis aut gyrum Arcturi poteris dissipare
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 numquid producis luciferum in tempore suo et vesperum super filios terrae consurgere facis
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 numquid nosti ordinem caeli et pones rationem eius in terra
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 numquid elevabis in nebula vocem tuam et impetus aquarum operiet te
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 numquid mittes fulgura et ibunt et revertentia dicent tibi adsumus
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 quis posuit in visceribus hominis sapientiam vel quis dedit gallo intellegentiam
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 quis enarravit caelorum rationem et concentum caeli quis dormire faciet
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 quando fundebatur pulvis in terram et glebae conpingebantur
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 numquid capies leaenae praedam et animam catulorum eius implebis
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 quando cubant in antris et in specubus insidiantur
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 quis praeparat corvo escam suam quando pulli eius ad Deum clamant vagantes eo quod non habeant cibos
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >