< Job 33 >
1 audi igitur Iob eloquia mea et omnes sermones meos ausculta
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 ecce aperui os meum loquatur lingua mea in faucibus meis
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 simplici corde meo sermones mei et sententiam labia mea puram loquentur
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 spiritus Dei fecit me et spiraculum Omnipotentis vivificavit me
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 si potes responde mihi et adversus faciem meam consiste
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 ecce et me sicut et te fecit Deus et de eodem luto ego quoque formatus sum
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 verumtamen miraculum meum non te terreat et eloquentia mea non sit tibi gravis
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 dixisti ergo in auribus meis et vocem verborum audivi
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 mundus sum ego absque delicto inmaculatus et non est iniquitas in me
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 quia querellas in me repperit ideo arbitratus est me inimicum sibi
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 posuit in nervo pedes meos custodivit omnes semitas meas
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 hoc est ergo in quo non es iustificatus respondebo tibi quia maior sit Deus homine
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 adversum eum contendis quod non ad omnia verba responderit tibi
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 semel loquitur Deus et secundo id ipsum non repetit
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 per somnium in visione nocturna quando inruit sopor super homines et dormiunt in lectulo
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 tunc aperit aures virorum et erudiens eos instruit disciplinam
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 ut avertat hominem ab his quae facit et liberet eum de superbia
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 eruens animam eius a corruptione et vitam illius ut non transeat in gladium
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 increpat quoque per dolorem in lectulo et omnia ossa eius marcescere facit
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 abominabilis ei fit in vita sua panis et animae illius cibus ante desiderabilis
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 tabescet caro eius et ossa quae tecta fuerant nudabuntur
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 adpropinquabit corruptioni anima eius et vita illius mortiferis
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 si fuerit pro eo angelus loquens unum de milibus ut adnuntiet hominis aequitatem
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 miserebitur eius et dicet libera eum et non descendat in corruptionem inveni in quo ei propitier
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 consumpta est caro eius a suppliciis revertatur ad dies adulescentiae suae
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 deprecabitur Deum et placabilis ei erit et videbit faciem eius in iubilo et reddet homini iustitiam suam
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 respiciet homines et dicet peccavi et vere deliqui et ut eram dignus non recepi
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 liberavit animam suam ne pergeret in interitum sed vivens lucem videret
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 ecce haec omnia operatur Deus tribus vicibus per singulos
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 ut revocet animas eorum a corruptione et inluminet luce viventium
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 adtende Iob et audi me et tace dum ego loquar
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 si autem habes quod loquaris responde mihi loquere volo enim te apparere iustum
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 quod si non habes audi me tace et docebo te sapientiam
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”