< Job 30 >
1 nunc autem derident me iuniores tempore quorum non dignabar patres ponere cum canibus gregis mei
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 quorum virtus manuum erat mihi pro nihilo et vita ipsa putabantur indigni
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 egestate et fame steriles qui rodebant in solitudine squalentes calamitate et miseria
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 et mandebant herbas et arborum cortices et radix iuniperorum erat cibus eorum
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 qui de convallibus ista rapientes cum singula repperissent ad ea cum clamore currebant
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 in desertis habitabant torrentium et in cavernis terrae vel super glaream
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 qui inter huiuscemodi laetabantur et esse sub sentibus delicias conputabant
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 filii stultorum et ignobilium et in terra penitus non parentes
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 nunc in eorum canticum versus sum et factus sum eis proverbium
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 abominantur me et longe fugiunt a me et faciem meam conspuere non verentur
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 faretram enim suam aperuit et adflixit me et frenum posuit in os meum
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 ad dexteram orientis calamitatis meae ilico surrexerunt pedes meos subverterunt et oppresserunt quasi fluctibus semitis suis
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 dissipaverunt itinera mea insidiati sunt mihi et praevaluerunt et non fuit qui ferret auxilium
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 quasi rupto muro et aperta ianua inruerunt super me et ad meas miserias devoluti sunt
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 redactus sum in nihili abstulisti quasi ventus desiderium meum et velut nubes pertransiit salus mea
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 nunc autem in memet ipso marcescit anima mea et possident me dies adflictionis
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 nocte os meum perforatur doloribus et qui me comedunt non dormiunt
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 in multitudine eorum consumitur vestimentum meum et quasi capitio tunicae sic cinxerunt me
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 conparatus sum luto et adsimilatus favillae et cineri
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 clamo ad te et non exaudis me sto et non respicis me
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 mutatus es mihi in crudelem et in duritia manus tuae adversaris mihi
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 elevasti me et quasi super ventum ponens elisisti me valide
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 scio quia morti tradas me ubi constituta domus est omni viventi
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 verumtamen non ad consumptionem eorum emittis manum tuam et si corruerint ipse salvabis
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 flebam quondam super eum qui adflictus erat et conpatiebatur anima mea pauperi
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 expectabam bona et venerunt mihi mala praestolabar lucem et eruperunt tenebrae
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 interiora mea efferbuerunt absque ulla requie praevenerunt me dies adflictionis
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 maerens incedebam sine furore consurgens in turba clamavi
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 frater fui draconum et socius strutionum
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 cutis mea denigrata est super me et ossa mea aruerunt prae caumate
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 versa est in luctum cithara mea et organum meum in vocem flentium
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.