< Job 29 >

1 addidit quoque Iob adsumens parabolam suam et dixit
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 quis mihi tribuat ut sim iuxta menses pristinos secundum dies quibus Deus custodiebat me
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 quando splendebat lucerna eius super caput meum et ad lumen eius ambulabam in tenebris
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 sicut fui in diebus adulescentiae meae quando secreto Deus erat in tabernaculo meo
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 quando erat Omnipotens mecum et in circuitu meo pueri mei
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 quando lavabam pedes meos butyro et petra fundebat mihi rivos olei
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 quando procedebam ad portam civitatis et in platea parabant cathedram mihi
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 videbant me iuvenes et abscondebantur et senes adsurgentes stabant
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 principes cessabant loqui et digitum superponebant ori suo
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 vocem suam cohibebant duces et lingua eorum gutturi suo adherebat
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 auris audiens beatificabat me et oculus videns testimonium reddebat mihi
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 quod liberassem pauperem vociferantem et pupillum cui non esset adiutor
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 benedictio perituri super me veniebat et cor viduae consolatus sum
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 iustitia indutus sum et vestivit me sicut vestimento et diademate iudicio meo
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 oculus fui caeco et pes claudo
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 pater eram pauperum et causam quam nesciebam diligentissime investigabam
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 conterebam molas iniqui et de dentibus illius auferebam praedam
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 dicebamque in nidulo meo moriar et sicut palma multiplicabo dies
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 radix mea aperta est secus aquas et ros morabitur in messione mea
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 gloria mea semper innovabitur et arcus meus in manu mea instaurabitur
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 qui me audiebant expectabant sententiam et intenti tacebant ad consilium meum
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 verbis meis addere nihil audebant et super illos stillabat eloquium meum
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 expectabant me sicut pluviam et os suum aperiebant quasi ad imbrem serotinum
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 si quando ridebam ad eos non credebant et lux vultus mei non cadebat in terram
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 si voluissem ire ad eos sedebam primus cumque sederem quasi rex circumstante exercitu eram tamen maerentium consolator
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Job 29 >