< Job 28 >
1 habet argentum venarum suarum principia et auro locus est in quo conflatur
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 ferrum de terra tollitur et lapis solutus calore in aes vertitur
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 tempus posuit tenebris et universorum finem ipse considerat lapidem quoque caliginis et umbram mortis
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 dividit torrens a populo peregrinante eos quos oblitus est pes egentis hominum et invios
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 terra de qua oriebatur panis in loco suo igne subversa est
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 locus sapphyri lapides eius et glebae illius aurum
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 semitam ignoravit avis nec intuitus est oculus vulturis
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 non calcaverunt eam filii institorum nec pertransivit per eam leaena
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 ad silicem extendit manum suam subvertit a radicibus montes
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 in petris rivos excidit et omne pretiosum vidit oculus eius
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 profunda quoque fluviorum scrutatus est et abscondita produxit in lucem
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 sapientia vero ubi invenitur et quis est locus intellegentiae
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 nescit homo pretium eius nec invenitur in terra suaviter viventium
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 abyssus dicit non est in me et mare loquitur non est mecum
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 non dabitur aurum obrizum pro ea nec adpendetur argentum in commutatione eius
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 non conferetur tinctis Indiae coloribus nec lapidi sardonico pretiosissimo vel sapphyro
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 non adaequabitur ei aurum vel vitrum nec commutabuntur pro ea vasa auri
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 excelsa et eminentia non memorabuntur conparatione eius trahitur autem sapientia de occultis
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 non adaequabitur ei topazium de Aethiopia nec tincturae mundissimae conponetur
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 unde ergo sapientia veniet et quis est locus intellegentiae
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 abscondita est ab oculis omnium viventium volucres quoque caeli latet
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 perditio et mors dixerunt auribus nostris audivimus famam eius
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 Deus intellegit viam eius et ipse novit locum illius
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 ipse enim fines mundi intuetur et omnia quae sub caelo sunt respicit
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 qui fecit ventis pondus et aquas adpendit mensura
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 quando ponebat pluviis legem et viam procellis sonantibus
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 tunc vidit illam et enarravit et praeparavit et investigavit
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 et dixit homini ecce timor Domini ipsa est sapientia et recedere a malo intellegentia
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”