< Job 26 >

1 respondens autem Iob dixit
Kisha Ayubu akajibu:
2 cuius adiutor es numquid inbecilli et sustentas brachium eius qui non est fortis
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 cui dedisti consilium forsitan illi qui non habet sapientiam et prudentiam tuam ostendisti plurimam
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 quem docere voluisti nonne eum qui fecit spiramen tuum
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 ecce gigantes gemunt sub aquis et qui habitant cum eis
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 nudus est inferus coram illo et nullum est operimentum perditioni (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 qui extendit aquilonem super vacuum et adpendit terram super nihili
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 qui ligat aquas in nubibus suis ut non erumpant pariter deorsum
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 qui tenet vultum solii sui et expandit super illud nebulam suam
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 terminum circumdedit aquis usque dum finiantur lux et tenebrae
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 columnae caeli contremescunt et pavent ad nutum eius
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 in fortitudine illius repente maria congregata sunt et prudentia eius percussit superbum
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 spiritus eius ornavit caelos et obsetricante manu eius eductus est coluber tortuosus
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 ecce haec ex parte dicta sunt viarum eius et cum vix parvam stillam sermonis eius audierimus quis poterit tonitruum magnitudinis illius intueri
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >