< Job 24 >
1 ab Omnipotente non sunt abscondita tempora qui autem noverunt eum ignorant dies illius
“Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
2 alii terminos transtulerunt diripuerunt greges et paverunt eos
Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
3 asinum pupillorum abigerunt et abstulerunt pro pignore bovem viduae
Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
4 subverterunt pauperum viam et oppresserunt pariter mansuetos terrae
Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
5 alii quasi onagri in deserto egrediuntur ad opus suum vigilantesque ad praedam praeparant panem liberis
Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
6 agrum non suum demetunt et vineam eius quem vi oppresserunt vindemiant
Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
7 nudos dimittunt homines indumenta tollentes quibus non est operimentum in frigore
Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
8 quos imbres montium rigant et non habentes velamen amplexantur lapides
Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
9 vim fecerunt depraedantes pupillos et vulgum pauperem spoliaverunt
Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
10 nudis et incedentibus absque vestitu et esurientibus tulerunt spicas
Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
11 inter acervos eorum meridiati sunt qui calcatis torcularibus sitiunt
Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
12 de civitatibus fecerunt viros gemere et anima vulneratorum clamavit et Deus inultum abire non patitur
Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
13 ipsi fuerunt rebelles luminis nescierunt vias eius nec reversi sunt per semitas illius
“Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
14 mane primo consurgit homicida interficit egenum et pauperem per noctem vero erit quasi fur
Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
15 oculus adulteri observat caliginem dicens non me videbit oculus et operiet vultum suum
Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
16 perfodit in tenebris domos sicut in die condixerant sibi et ignoraverunt lucem
Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
17 si subito apparuerit aurora arbitrantur umbram mortis et sic in tenebris quasi in luce ambulant
Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
18 levis est super faciem aquae maledicta sit pars eius in terra nec ambulet per viam vinearum
“Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
19 ad nimium calorem transeat ab aquis nivium et usque ad inferos peccatum illius (Sheol )
Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol )
20 obliviscatur eius misericordia dulcedo illius vermes non sit in recordatione sed conteratur quasi lignum infructuosum
Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
21 pavit enim sterilem et quae non parit et viduae bene non fecit
Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
22 detraxit fortes in fortitudine sua et cum steterit non credet vitae suae
Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
23 dedit ei Deus locum paenitentiae et ille abutitur eo in superbiam oculi autem eius sunt in viis illius
Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
24 elevati sunt ad modicum et non subsistent et humiliabuntur sicut omnia et auferentur et sicut summitates spicarum conterentur
Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
25 quod si non est ita quis me potest arguere esse mentitum et ponere ante Deum verba mea
“Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”