< Job 18 >
1 respondens autem Baldad Suites dixit
Bildadi Mshuhi akajibu:
2 usque ad quem finem verba iactabitis intellegite prius et sic loquamur
“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3 quare reputati sumus ut iumenta et sorduimus coram vobis
Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4 qui perdis animam tuam in furore tuo numquid propter te derelinquetur terra et transferentur rupes de loco suo
Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5 nonne lux impii extinguetur nec splendebit flamma ignis eius
“Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6 lux obtenebrescet in tabernaculo illius et lucerna quae super eum est extinguetur
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7 artabuntur gressus virtutis eius et praecipitabit eum consilium suum
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8 inmisit enim in rete pedes suos et in maculis eius ambulat
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 tenebitur planta illius laqueo et exardescet contra eum sitis
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 abscondita est in terra pedica eius et decipula illius super semitam
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11 undique terrebunt eum formidines et involvent pedes eius
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12 adtenuetur fame robur eius et inedia invadat costas illius
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 devoret pulchritudinem cutis eius consumat brachia illius primogenita mors
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 avellatur de tabernaculo suo fiducia eius et calcet super eum quasi rex interitus
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 habitent in tabernaculo illius socii eius qui non est aspergatur in tabernaculo eius sulphur
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16 deorsum radices eius siccentur sursum autem adteratur messis eius
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17 memoria illius pereat de terra et non celebretur nomen eius in plateis
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18 expellet eum de luce in tenebras et de orbe transferet eum
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19 non erit semen eius neque progenies in populo suo nec ullae reliquiae in regionibus eius
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20 in die eius stupebunt novissimi et primos invadet horror
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21 haec sunt ergo tabernacula iniqui et iste locus eius qui ignorat Deum
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”