< Job 14 >
1 homo natus de muliere brevi vivens tempore repletus multis miseriis
Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
2 quasi flos egreditur et conteritur et fugit velut umbra et numquam in eodem statu permanet
Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
3 et dignum ducis super huiuscemodi aperire oculos tuos et adducere eum tecum in iudicium
Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
4 quis potest facere mundum de inmundo conceptum semine nonne tu qui solus es
Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
5 breves dies hominis sunt numerus mensuum eius apud te est constituisti terminos eius qui praeterire non poterunt
Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
6 recede paululum ab eo ut quiescat donec optata veniat sicut mercennarii dies eius
Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
7 lignum habet spem si praecisum fuerit rursum virescit et rami eius pullulant
Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
8 si senuerit in terra radix eius et in pulvere emortuus fuerit truncus illius
Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
9 ad odorem aquae germinabit et faciet comam quasi cum primum plantatum est
hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
10 homo vero cum mortuus fuerit et nudatus atque consumptus ubi quaeso est
Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
11 quomodo si recedant aquae de mari et fluvius vacuefactus arescat
Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
12 sic homo cum dormierit non resurget donec adteratur caelum non evigilabit nec consurget de somno suo
vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
13 quis mihi hoc tribuat ut in inferno protegas me ut abscondas me donec pertranseat furor tuus et constituas mihi tempus in quo recorderis mei (Sheol )
Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol )
14 putasne mortuus homo rursum vivet cunctis diebus quibus nunc milito expecto donec veniat inmutatio mea
Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
15 vocabis et ego respondebo tibi operi manuum tuarum porriges dexteram
Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
16 tu quidem gressus meos dinumerasti sed parces peccatis meis
Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
17 signasti quasi in sacculo delicta mea sed curasti iniquitatem meam
Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
18 mons cadens defluet et saxum transfertur de loco suo
Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
19 lapides excavant aquae et adluvione paulatim terra consumitur et homines ergo similiter perdes
maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
20 roborasti eum paululum ut in perpetuum pertransiret inmutabis faciem eius et emittes eum
Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
21 sive nobiles fuerint filii eius sive ignobiles non intelleget
Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
22 attamen caro eius dum vivet dolebit et anima illius super semet ipso lugebit
Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.