< Job 14 >
1 homo natus de muliere brevi vivens tempore repletus multis miseriis
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 quasi flos egreditur et conteritur et fugit velut umbra et numquam in eodem statu permanet
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 et dignum ducis super huiuscemodi aperire oculos tuos et adducere eum tecum in iudicium
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 quis potest facere mundum de inmundo conceptum semine nonne tu qui solus es
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 breves dies hominis sunt numerus mensuum eius apud te est constituisti terminos eius qui praeterire non poterunt
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 recede paululum ab eo ut quiescat donec optata veniat sicut mercennarii dies eius
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 lignum habet spem si praecisum fuerit rursum virescit et rami eius pullulant
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 si senuerit in terra radix eius et in pulvere emortuus fuerit truncus illius
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 ad odorem aquae germinabit et faciet comam quasi cum primum plantatum est
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 homo vero cum mortuus fuerit et nudatus atque consumptus ubi quaeso est
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 quomodo si recedant aquae de mari et fluvius vacuefactus arescat
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 sic homo cum dormierit non resurget donec adteratur caelum non evigilabit nec consurget de somno suo
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
13 quis mihi hoc tribuat ut in inferno protegas me ut abscondas me donec pertranseat furor tuus et constituas mihi tempus in quo recorderis mei (Sheol )
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol )
14 putasne mortuus homo rursum vivet cunctis diebus quibus nunc milito expecto donec veniat inmutatio mea
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 vocabis et ego respondebo tibi operi manuum tuarum porriges dexteram
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 tu quidem gressus meos dinumerasti sed parces peccatis meis
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 signasti quasi in sacculo delicta mea sed curasti iniquitatem meam
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 mons cadens defluet et saxum transfertur de loco suo
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 lapides excavant aquae et adluvione paulatim terra consumitur et homines ergo similiter perdes
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 roborasti eum paululum ut in perpetuum pertransiret inmutabis faciem eius et emittes eum
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 sive nobiles fuerint filii eius sive ignobiles non intelleget
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
22 attamen caro eius dum vivet dolebit et anima illius super semet ipso lugebit
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”