< Genesis 10 >

1 hae generationes filiorum Noe Sem Ham Iafeth natique sunt eis filii post diluvium
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 filii Iafeth Gomer Magog et Madai Iavan et Thubal et Mosoch et Thiras
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 porro filii Gomer Aschenez et Rifath et Thogorma
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 filii autem Iavan Elisa et Tharsis Cetthim et Dodanim
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 ab his divisae sunt insulae gentium in regionibus suis unusquisque secundum linguam et familias in nationibus suis
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 filii autem Ham Chus et Mesraim et Fut et Chanaan
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 filii Chus Saba et Hevila et Sabatha et Regma et Sabathaca filii Regma Saba et Dadan
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 porro Chus genuit Nemrod ipse coepit esse potens in terra
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 et erat robustus venator coram Domino ab hoc exivit proverbium quasi Nemrod robustus venator coram Domino
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 fuit autem principium regni eius Babylon et Arach et Archad et Chalanne in terra Sennaar
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 de terra illa egressus est Assur et aedificavit Nineven et plateas civitatis et Chale
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 Resen quoque inter Nineven et Chale haec est civitas magna
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 at vero Mesraim genuit Ludim et Anamim et Laabim Nepthuim
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 et Phetrusim et Cesluim de quibus egressi sunt Philisthim et Capthurim
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Chanaan autem genuit Sidonem primogenitum suum Ettheum
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 et Iebuseum et Amorreum Gergeseum
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Eveum et Araceum Sineum
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 et Aradium Samariten et Amatheum et post haec disseminati sunt populi Chananeorum
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 factique sunt termini Chanaan venientibus a Sidone Geraram usque Gazam donec ingrediaris Sodomam et Gomorram et Adama et Seboim usque Lesa
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 hii filii Ham in cognationibus et linguis et generationibus terrisque et gentibus suis
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 de Sem quoque nati sunt patre omnium filiorum Eber fratre Iafeth maiore
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 filii Sem Aelam et Assur et Arfaxad et Lud et Aram
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 filii Aram Us et Hul et Gether et Mes
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 at vero Arfaxad genuit Sala de quo ortus est Eber
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 natique sunt Eber filii duo nomen uni Faleg eo quod in diebus eius divisa sit terra et nomen fratris eius Iectan
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 qui Iectan genuit Helmodad et Saleph et Asarmoth Iare
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 et Aduram et Uzal Decla
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 et Ebal et Abimahel Saba
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 et Ophir et Evila et Iobab omnes isti filii Iectan
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 et facta est habitatio eorum de Messa pergentibus usque Sephar montem orientalem
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 isti filii Sem secundum cognationes et linguas et regiones in gentibus suis
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 hae familiae Noe iuxta populos et nationes suas ab his divisae sunt gentes in terra post diluvium
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< Genesis 10 >