< Deuteronomii 27 >

1 praecepit autem Moses et seniores Israhel populo dicentes custodite omne mandatum quod praecipio vobis hodie
Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
2 cumque transieritis Iordanem in terram quam Dominus Deus tuus dabit tibi eriges ingentes lapides et calce levigabis eos
Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
3 ut possis in eis scribere omnia verba legis huius Iordane transmisso ut introeas terram quam Dominus Deus tuus dabit tibi terram lacte et melle manantem sicut iuravit patribus tuis
Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
4 quando ergo transieritis Iordanem erige lapides quos ego hodie praecipio vobis in monte Hebal et levigabis calce
Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
5 et aedificabis ibi altare Domino Deo tuo de lapidibus quos ferrum non tetigit
Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
6 et de saxis informibus et inpolitis et offeres super eo holocausta Domino Deo tuo
Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
7 et immolabis hostias pacificas comedesque ibi et epulaberis coram Domino Deo tuo
Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
8 et scribes super lapides omnia verba legis huius plane et lucide
Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
9 dixeruntque Moses et sacerdotes levitici generis ad omnem Israhelem adtende et audi Israhel hodie factus es populus Domini Dei tui
Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
10 audies vocem eius et facies mandata atque iustitias quas ego praecipio tibi
Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
11 praecepitque Moses populo in die illo dicens
Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
12 hii stabunt ad benedicendum Domino super montem Garizim Iordane transmisso Symeon Levi Iudas Isachar Ioseph et Beniamin
Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
13 et e regione isti stabunt ad maledicendum in monte Hebal Ruben Gad et Aser Zabulon Dan et Nepthalim
Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
14 et pronuntiabunt Levitae dicentque ad omnes viros Israhel excelsa voce
Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 maledictus homo qui facit sculptile et conflatile abominationem Domini opus manuum artificum ponetque illud in abscondito et respondebit omnis populus et dicet amen
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16 maledictus qui non honorat patrem suum et matrem et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17 maledictus qui transfert terminos proximi sui et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18 maledictus qui errare facit caecum in itinere et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19 maledictus qui pervertit iudicium advenae pupilli et viduae et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20 maledictus qui dormit cum uxore patris sui et revelat operimentum lectuli eius et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21 maledictus qui dormit cum omni iumento et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22 maledictus qui dormit cum sorore sua filia patris sui sive matris suae et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23 maledictus qui dormit cum socru sua et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24 maledictus qui clam percusserit proximum suum et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25 maledictus qui accipit munera ut percutiat animam sanguinis innocentis et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26 maledictus qui non permanet in sermonibus legis huius nec eos opere perficit et dicet omnis populus amen
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

< Deuteronomii 27 >