< Psalmorum 91 >
1 Laus Cantici David. Qui habitat in adiutorio Altissimi, in protectione Dei caeli commorabitur.
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
2 Dicet Domino: Susceptor meus es tu, et refugium meum: Deus meus sperabo in eum.
Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
3 Quoniam ipse liberavit me de laqueo venantium, et a verbo aspero.
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4 Scapulis suis obumbrabit tibi: et sub pennis eius sperabis:
Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5 Scuto circumdabit te veritas eius: non timebis a timore nocturno,
Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
6 A sagitta volante in die, a negotio perambulante in tenebris: ab incursu, et daemonio meridiano.
wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7 Cadent a latere tuo mille, et decem millia a dextris tuis: ad te autem non appropinquabit.
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
8 Verumtamen oculis tuis considerabis: et retributionem peccatorum videbis.
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
9 Quoniam tu es Domine spes mea: Altissimum posuisti refugium tuum.
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10 Non accedet ad te malum: et flagellum non appropinquabit tabernaculo tuo.
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
11 Quoniam angelis suis mandavit de te: ut custodiant te in omnibus viis tuis.
Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
12 In manibus portabunt te: ne forte offendas ad lapidem pedem tuum.
Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13 Super aspidem, et basiliscum ambulabis: et conculcabis leonem et draconem.
Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
14 Quoniam in me speravit, liberabo eum: protegam eum, quoniam cognovit nomen meum.
Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
15 Clamabit ad me, et ego exaudiam eum: cum ipso sum in tribulatione: eripiam eum et glorificabo eum.
Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
16 Longitudine dierum replebo eum: et ostendam illi salutare meum.
Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”