< Psalmorum 88 >

1 Psalmus, Canticum psalmi, in finem, filiis Core, pro Maheleth ad respondendum, intellectus Eman Israelitae. Domine Deus salutis meae: in die clamavi, et nocte coram te.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Intret in conspectu tuo oratio mea: inclina aurem tuam ad precem meam:
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 Quia repleta est malis anima mea: et vita mea inferno appropinquavit. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 Aestimatus sum cum descendentibus in lacum: factus sum sicut homo sine adiutorio,
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 inter mortuos liber, Sicut vulnerati dormientes in sepulchris, quorum non es memor amplius: et ipsi de manu tua repulsi sunt.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Posuerunt me in lacu inferiori: in tenebrosis, et in umbra mortis.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Super me confirmatus est furor tuus: et omnes fluctus tuos induxisti super me.
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Longe fecisti notos meos a me: posuerunt me abominationem sibi. Traditus sum, et non egrediebar:
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 oculi mei languerunt prae inopia. Clamavi ad te Domine tota die: expandi ad te manus meas.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 Numquid mortuis facies mirabilia: aut medici suscitabunt, et confitebuntur tibi?
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 Numquid narrabit aliquis in sepulchro misericordiam tuam, et veritatem tuam in perditione?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 Numquid cognoscentur in tenebris mirabilia tua: et iustitia tua in terra oblivionis?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 Et ego ad te, Domine, clamavi, et mane oratio mea praeveniet te.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 Ut quid Domine repellis orationem meam: avertis faciem tuam a me?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 Pauper sum ego, et in laboribus a iuventute mea: exaltatus autem, humiliatus sum et conturbatus.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 In me transierunt irae tuae: et terrores tui conturbaverunt me.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 Circumdederunt me sicut aqua tota die: circumdederunt me simul.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Elongasti a me amicum, et proximum: et notos meos a miseria.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Psalmorum 88 >