< Psalmorum 77 >

1 Psalmus Asaph, in finem, pro Idithum. Voce mea ad Dominum clamavi: voce mea ad Deum, et intendit mihi.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 In die tribulationis meae Deum exquisivi, manibus meis nocte contra eum: et non sum deceptus. Renuit consolari anima mea,
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 memor fui Dei, et delectatus sum, et exercitatus sum: et defecit spiritus meus.
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Anticipaverunt vigilias oculi mei: turbatus sum, et non sum locutus.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 Cogitavi dies antiquos: et annos aeternos in mente habui.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 Et meditatus sum nocte cum corde meo, et exercitabar, et scopebam spiritum meum.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 Numquid in aeternum proiiciet Deus: aut non apponet ut complacitior sit adhuc?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Aut in finem misericordiam suam abscindet, a generatione in generationem?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Aut obliviscetur misereri Deus? aut continebit in ira sua misericordias suas?
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 Et dixi nunc coepi: haec mutatio dexterae Excelsi.
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 Memor fui operum Domini: quia memor ero ab initio mirabilium tuorum,
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 Et meditabor in omnibus operibus tuis: et in adinventionibus tuis exercebor.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Deus in sancto via tua: quis Deus magnus sicut Deus noster?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 tu es Deus qui facis mirabilia. Notam fecisti in populis virtutem tuam:
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 redemisti in brachio tuo populum tuum, filios Iacob, et Ioseph.
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 Viderunt te aquae Deus, viderunt te aquae: et timuerunt, et turbatae sunt abyssi.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 Multitudo sonitus aquarum: vocem dederunt nubes. Etenim sagittae tuae transeunt:
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 vox tonitrui tui in rota. Illuxerunt coruscationes tuae orbi terrae: commota est et contremuit terra.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 In mari via tua, et semitae tuae in aquis multis: et vestigia tua non cognoscentur.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Deduxisti sicut oves populum tuum, in manu Moysi et Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< Psalmorum 77 >