< Psalmorum 62 >

1 Psalmus David, in finem, pro Idithum. Nonne Deo subiecta erit anima mea? ab ipso enim salutare meum.
Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
2 Nam et ipse Deus meus, et salutaris meus: susceptor meus, non movebor amplius.
Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
3 Quousque irruitis in hominem? interficitis universi vos: tamquam parieti inclinato et maceriae depulsae.
Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
4 Verumtamen pretium meum cogitaverunt repellere, cucurri in siti: ore suo benedicebant, et corde suo maledicebant.
Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
5 Verumtamen Deo subiecta esto anima mea: quoniam ab ipso patientia mea.
Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
6 Quia ipse Deus meus, et salvator meus: adiutor meus, non emigrabo.
Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
7 In Deo salutare meum, et gloria mea: Deus auxilii mei, et spes mea in Deo est.
Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
8 Sperate in eo omnis congregatio populi, effundite coram illo corda vestra: Deus adiutor noster in aeternum.
Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
9 Verumtamen vani filii hominum, mendaces filii hominum in stateris: ut decipiant ipsi de vanitate in idipsum.
Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
10 Nolite sperare in iniquitate, et rapinas nolite concupiscere: divitiae si affluant, nolite cor apponere.
Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
11 Semel locutus est Deus, duo haec audivi, quia potestas Dei est,
Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
12 et tibi Domine misericordia: quia tu reddes unicuique iuxta opera sua.
Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.

< Psalmorum 62 >